Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yona 2:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Niliteremuka mpaka kwenye misingi ya milima, katika inchi ambayo milango yake imefungwa milele. Lakini wewe, ee Yawe, Mungu wangu, umenipandisha nikiwa muzima kutoka mule ndani ya shimo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yona 2:7
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha, makuhani na Walawi wakawaombea watu baraka za Yawe, naye katika makao yake matakatifu kule mbinguni akasikia maombi yao na kuyakubali.


Yawe yuko katika hekalu lake takatifu; kiti cha kifalme cha Yawe kiko mbinguni. Kwa macho yake anawachungulia wanadamu, na kujua kila kitu wanachofanya.


Ninamutolea malalamiko yangu, ninamwelezea taabu zangu.


Ninakumbuka siku za zamani, ninafikiri juu ya yote uliyotenda, ninawazawaza matendo yako.


kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya kifo ilikuwa mbele yangu.


Ninajua Yawe atamusaidia mufalme aliyemuchagua, atamujibu tokea pahali pake patakatifu mbinguni; kwa mukono wake wenye nguvu atamujalia ushindi mukubwa.


Wanafungua vinywa vyao kama simba, tayari kushambulia na kurarua.


Ninaamini kwamba nitauona uzuri wa Yawe katika makao ya wazima.


Nimepondekana kwa ajili ya matukano yao, wanaponiuliza kila siku: “Mungu wako, yupo wapi?”


Katika huzuni yangu, ninakumbuka jinsi nilivyokwenda na kundi la watu na kuwaongoza kwenda katika nyumba ya Mungu wakipiga vigelegele vya shukrani, kundi la watu likifanya sherehe!


Mbona ninahuzunika hivyo katika moyo? Kwa nini ninahangaika hivyo ndani mwangu? Nitamutumainia Mungu, nitamusifu tena yeye anayekuwa musaada wangu na Mungu wangu.


Tunapolemewa na makosa yetu, wewe mwenyewe unatusamehe.


Nilipata mateso makali kwa faida yangu; lakini umeyaokoa maisha yangu kutoka shimo la uharibifu, maana umezitupa zambi zangu nyuma yako.


Nani kati yenu anayemwogopa Yawe? Nani anayetii maneno ya mutumishi wake? Kama kuna mutu anayetembea katika giza bila taa, amutumainie Yawe, na kumutegemea Mungu wake.


Ulinitupa katika kilindi, katikati ya bahari, maji mengi yakanizunguka, mawimbi na maji mengi vikapita juu yangu.


Musikilize enyi watu wote; sikiliza ewe dunia na vyote vinavyokuwa ndani yako. Bwana wetu Yawe anakuja kuwashitaki, Bwana wetu anasema kutoka hekalu lake takatifu.


Lakini Yawe yuko katika hekalu lake takatifu; dunia yote ikae kimya mbele yake.


Kwa hiyo mumukumbuke yule aliyevumilia kutendewa na wenye zambi kwa chuki kubwa, kusudi musipate kuchoka wala kuregea.


Sasa, Daudi alikuwa katika matatizo makubwa kwa sababu watu wake walikuwa na uchungu katika roho zao kwa kupoteza watoto wao. Kwa hiyo wakakuwa wakitaka kumupiga mawe. Lakini Daudi alijipa moyo kwa kumutegemea Yawe, Mungu wake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ