Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yona 2:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Maji yalinizunguka na kunisonga; kilindi kilinifikia kila upande, majani ya bahari yakanifunika kichwa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yona 2:6
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yule malaika anaweza kumwonea huruma na kumwomba Mungu: “Umwokoe asiingie katika shimo; nimepata ukombozi wake.”


Mungu aliniokoa nisiangamie katika shimo; nimebaki muzima na ninaona mwangaza.”


Uliifunika dunia kwa bahari kama nguo, na maji yakaimeza milima mirefu.


Yaliporomoka toka milima mpaka katika mabonde, mpaka pahali ulipoyatengenezea.


Hatari ya kifo ilinizunguka, vitisho vya kaburi vilinishika; nilisongwa na mahangaiko na huzuni.


Ee Yawe, unijibu haraka; maana roho yangu imeregea kabisa! Usinigeuzie mugongo, kusudi nisikuwe kama wale wanaoshuka katika shimo la wafu.


Kweli wewe unanikinga na nguvu za kuzimu, haumwachi mutakatifu wako aone kaburi.


Kamba za kifo zilinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinishambulia;


Ee Yawe, Mungu wangu, nilikulilia, nawe ukaniponyesha.


Nilikulilia wewe, ee Yawe; nilikusihi, ee Yawe:


Utue muzigo wako kwa Yawe, naye atakusaidia; hamwachilii mutu wa haki ashindwe.


Kwa matendo yako makubwa unatuitikia na kutuokoa, ewe Mungu mwokozi wetu. Wewe ndiwe tumaini la viumbe vyote katika dunia yote na mbali katika bahari.


Uniokoe, ee Mungu; maji yamenifikia katika shingo.


Nilisema: nikiwa mubichi kabisa, inanipasa niage dunia. Mimi nimepangiwa kwenda katika kuzimu siku zote zilizonibakilia.


Nilipata mateso makali kwa faida yangu; lakini umeyaokoa maisha yangu kutoka shimo la uharibifu, maana umezitupa zambi zangu nyuma yako.


Ni nani anayeweza kupima maji ya bahari katika kitanga cha mukono wake, na kuzipima mbingu kwa mikono yake? Ni nani anayeweza kuutia udongo wa dunia katika kikombe; kuipima milima kwa mizani au vilima kwa kipimo cha uzito?


Nitakuteremusha ndani ya shimo kusudi ujiunge na wale wanaokuwa huko, walioishi zamani katika dunia; utakaa kule katika matongo kwa milele. Hautakaliwa na watu milele na hautakuwa na nafasi katika inchi za wanaokuwa wazima.


Hayo yameupata kusudi muti wowote unaokuwa pahali penye maji usiweze kurefuka tena kwa kimo hicho wala kukifikisha kilele chake katika mawingu. Muti wowote unaokunyweshwa maji usiweze tena kufikia urefu huo. Kwa maana kila kitu mwisho wake ni kifo; hata na watu vilevile. Wote watashiriki hali ya wanaoshuka katika shimo kwa wafu.


Milima ilikuona, ikanyauka; mafuriko ya maji yakapita mule. Vilindi vya bahari vilinguruma, na kurusha juu mawimbi yake.


Akisimama dunia inatikisika; akiyatupia mataifa jicho, hayo yanatetemeka. Milima ya milele inavunjwavunjwa, vilima vya zamani za kale vinaanguka; ni juu yao kulipokuwa njia zake za kale na kale.


Nami sasa ninakuambia: ewe Petro, wewe ni jiwe, na juu ya jiwe hili, nitajenga musingi wa kanisa langu, na hata uwezo wa lufu hautaweza kulishinda.


Hasira yangu imewaka moto, inachoma mpaka chini kuzimu, itateketeza dunia na vinavyokuwa ndani yake, itaunguza misingi ya milima.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ