Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yona 1:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Watumishi wa mashua wakaogopa, kila mumoja akaanza kumulilia mungu wake. Wakatupa katika bahari mizigo yote kwa kupunguza uzito wa mashua. Wakati ule, Yona alikuwa ameshuka katika sehemu ya ndani ya mashua, akalala usingizi muzito.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yona 1:5
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hao manabii wakamutwaa ngombe dume wao waliyepewa, wakamutayarisha, kisha wakaanza kumulilia Bali kutokea asubui mpaka saa sita za muchana, wakirukaruka pembeni ya mazabahu waliyotengeneza wakisema: “Ee Bali, utusikilize!” Lakini hakukutokea sauti yoyote, wala hakuna aliyewajibu.


Shetani akamujibu Yawe: “Ngozi kwa ngozi! Mutu anatoa kila kitu anachokuwa nacho kusudi aokoe maisha yake.


Aliamuru, akavumisha zoruba kali, ikarusha juu mawimbi ya bahari.


Mumusifu, enyi moto, mvua ya mawe na teluji, upepo wenye zoruba unaotimiza amri yake!


wakati wa kutafuta na wakati wa kupoteza, wakati wa kuchunga na wakati wa kutupa,


Enyi watu wa mataifa muliobaki, mukusanyike pamoja mukuje! Ninyi mumekosa akili: ninyi munabeba sanamu za miti na kumwomba mungu asiyeweza kuokoa watu.


Lakini iko wapi ile miungu yenu muliyojifanyia? Basi kama inaweza, isimame iwasaidie, wakati munapokuwa katika shida. Ee ninyi watu wa Yuda, hesabu ya miungu yenu ni sawa na hesabu ya miji yenu!


Wananililia, lakini si kwa moyo. Wanagaagaa na kujikatakata juu ya vitanda vyao, kusudi nisikilize maombi yao kwa kupata ngano na divai; lakini wanaendelea kuniasi.


Basi, wakamulilia Yawe wakisema: Ee Yawe, tunakusihi usituangamize kwa kuutoa uzima wa mutu huyu, wala usituazibu kwa kumwanga damu ya mutu asiyekuwa na kosa. Wewe, ee Yawe, umefanya unavyopenda.


Watu hao wakamwogopa sana Yawe, wakamutolea sadaka na kufanya viapo.


Kapiteni wa mashua akamwendea, akamwambia: Namna gani wewe unaweza kulala? Amuka umwombe Mungu wako; labda Mungu wako atatuhurumia na kuyaokoa maisha yetu.


Na kwa kuona bwana-arusi alikawia kufika, wote wakasinzia na kulala usingizi.


Aliporudi tena, akawakuta wanafunzi wale wamelala usingizi, kwa maana macho yao yalikuwa yamewezwa sana na usingizi.


Kisha akarudi kwenye wanafunzi wake na kuwaambia: “Mungali munalala na kupumzika? Angalia, saa imetimia, sasa Mwana wa Mutu anatolewa katika mikono ya wenye zambi.


Walipokwisha kushiba, wakatupa mizigo ya ngano katika bahari kwa kupunguza uzito wa chombo.


Naye Delila akamufanya Samusoni alale usingizi juu ya magoti yake, akamwita mutu amunyoe ile misuko yake saba. Kisha Delila akaanza kumutesa Samusoni kwa sababu sasa nguvu zilikuwa zimemutoka.


Kisha Saulo aliwatwaa waaskari elfu tatu waliochaguliwa waliokuwa bora zaidi katika inchi yote ya Israeli, akaenda kumutafuta Daudi na watu wake pahali panapoitwa “Mawe ya Mbuzi wa Pori.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ