13 Watumishi wale wakajaribu kuvuta makasia wapate kuifikisha mashua yao inchi kavu, lakini hawakufanikiwa kwa maana bahari ilizidi kuwachafukia.
Kama Mungu akinyamaza, nani anayeweza kumuhukumu? Kama akificha uso wake, nani anayeweza kumwona, ikiwa ni taifa au mutu mumoja?
Hakuna hekima, ufahamu, wala shauri yoyote ya mutu, itakayoweza kupingana na Yawe.
Yona akawajibu: Munikamate na kunitupa katika bahari, nayo bahari itatulia, maana ninaona wazi kwamba zoruba hii imewapata kwa sababu yangu mimi.
Basi, wakamulilia Yawe wakisema: Ee Yawe, tunakusihi usituangamize kwa kuutoa uzima wa mutu huyu, wala usituazibu kwa kumwanga damu ya mutu asiyekuwa na kosa. Wewe, ee Yawe, umefanya unavyopenda.