Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yona 1:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Yona akawajibu: Munikamate na kunitupa katika bahari, nayo bahari itatulia, maana ninaona wazi kwamba zoruba hii imewapata kwa sababu yangu mimi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yona 1:12
10 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Daudi alipomwona yule malaika aliyekuwa anawaua watu, alimwambia, Yawe: “Mimi ndiye ninayekuwa na kosa! Mimi mwenyewe nimekosa! Hawa watu wapole hawakufanya uovu. Ninakusihi sana uniazibu mimi na jamaa ya baba yangu.”


Daudi akamwambia Mungu: “Si mimi ndiye niliyetoa amri watu wahesabiwe? Ni mimi niliyetenda zambi na kufanya uovu. Lakini kondoo hawa wamefanya nini? Ninakusihi sana, ee Yawe, Mungu wangu, mukono wako ukuwe juu yangu na juu ya jamaa ya baba yangu, lakini ugonjwa huu mukali usiwapate watu wako.”


Uovu wako utamuzuru mwanadamu kama wewe, haki yako itamufalia mwanadamu mwenzako.


Kuwa na hekima ni bora kuliko kutegemea silaha, lakini mwenye zambi mumoja anaharibu mazuri mengi.


Wakati huo wote, bahari ilikuwa inazidi kuchafuka. Basi, wakamwuliza Yona: Tukufanye nini kusudi bahari itulie?


Watumishi wale wakajaribu kuvuta makasia wapate kuifikisha mashua yao inchi kavu, lakini hawakufanikiwa kwa maana bahari ilizidi kuwachafukia.


Hamufahamu kwamba ni afazali mutu mumoja akufe kwa ajili ya watu, kuliko taifa zima kuangamizwa?”


na kuniambia: ‘Paulo, usiogope! Sherti usambe mbele ya Mufalme wa Roma. Na tena kwa kuwa inamupendeza Mungu kukutendea mema, yeye ataokoa maisha ya watu hawa wote wanaosafiri pamoja nawe.’


Kwa hiyo Waisraeli hawawezi kuwashinda waadui zao. Wanawakimbia waadui zao kwa sababu wamejifanya wenyewe kuwa kitu cha kuangamizwa! Sitakuwa pamoja nao tena musipoharibu vitu vinavyokuwa kati yenu vilivyotolewa viangamizwe.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ