Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya makosa matatu ya Waisraeli, hata kwa mane, sitageuza nia yangu. Wameuzisha watu wa haki kuwa watumwa kwa maana hawakuweza kulipa madeni yao; na kuwauzisha wakosefu wanaoshindwa kulipa deni la muguu mumoja wa mapapa.
Siku ile mulisimama pembeni mukiangalia tu, wakati wageni walipouteka utajiri wao, walipoingia katika milango yake na kugawanya utajiri wa Yerusalema kwa kupiga kura. Nanyi vilevile mulikuwa kama wamoja wao.
Hata hivyo, ulikamatwa mateka, watu wake wakapelekwa katika uhamisho. Hata watoto wake walipondwapondwa katika maingilio ya kila barabara; watu wake wenye heshima waligawanywa kwa kuwapigia kura, wakubwa wake wote walifungwa minyororo.