Yoeli 2:27 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
27 Mutatambua kwamba mimi niko kati yenu, enyi Waisraeli; na kwamba mimi Yawe, ndimi Mungu wenu wala hakuna mwingine. Watu wangu, hawatazarauliwa tena hata kidogo.
Nitaimwangilia maji inchi yenye kiu, na kutiririsha muto katika inchi iliyokauka. Nitajaza roho wangu juu ya wazao wako, nitawamwangia watoto wako baraka yangu.
Enyi watu wangu, musiogope wala musikuwe na hofu, Sikuwaambia tangu zamani mambo yatakayotokea? Ninyi ni washuhuda wangu. Kuna mungu mwingine isipokuwa mimi? Kuna mwenye nguvu mwingine? Yule simujui!
Hivi ndivyo anavyosema Yawe aliyeumba mbingu, ndiye Mungu aliyeipa dunia umbo na kuifanya na kuiimarisha. Hakuiumba kusudi ibaki ukiwa, lakini aliipa umbo kusudi iikaliwe na viumbe vyake: Mimi ni Yawe, wala hakuna mwingine.
Wafalme watakushugulikia, na malkia watakutengenezea chakula. Watainama mbele yako uso mpaka chini, na kulambula mavumbi ya miguu yako. Halafu utatambua kwamba mimi ni Yawe; wote wanaonitegemea hawatapata haya.
Kisha watatambua kwamba mimi ni Yawe, Mungu wao, kwa sababu mimi niliwapeleka katika uhamisho kati ya mataifa na kuwarudisha tena katika inchi yao. Sitamwacha hata mutu wao mumoja abakie kati ya mataifa.
Siku hiyo, hautapata haya kutokana na matendo yako ya kuniasi, maana nitawaondoa kati yako wale wanaojivuna na kujitukuza, nawe hautakuwa na kiburi tena kwenye mulima wangu mutakatifu.
Yawe, Mungu wako, yuko pamoja nawe. Yeye ni shujaa anayekuletea ushindi. Yeye atakufurahia kwa furaha kubwa. Kwa upendo wake atakujalia uzima mupya. Atakufurahia kwa wimbo wa sauti kubwa,
Yawe hajaona ubaya kwa watu wa Yakobo, wala uovu kwa hao watu wa Israeli. Yawe Mungu wao yuko pamoja nao, Yeye anasifiwa kwa vigelegele kati yao, yeye anapokea sifa zao za kifalme.
Kuna ulinganisho gani kati ya hekalu la Mungu na sanamu? Kwa maana sisi ni hekalu la Mungu Mwenye Uzima kama vile yeye mwenyewe alivyosema: “Nitakaa na kuishi pamoja nao, nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.”
Kwa kuwa imeandikwa hivi katika Maandiko Matakatifu: “Nimesimika jiwe kubwa la pembe katika Sayuni, jiwe lile ni la bei kali. Ni mimi niliyelichagua. Yule anayelitumainia hatapata haya.”
Nikasikia sauti kubwa tokea kwenye kiti cha kifalme ikisema: “Sasa makao ya Mungu yanapatikana kati ya watu! Yeye atakaa pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao, naye atakuwa Mungu wao.