Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoeli 2:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

23 Mufurahi, enyi watu wa Sayuni, mushangilie kwa sababu ya Yawe, Mungu wenu, maana amewapa mvua zinazowafalia, amewapa mvua ya kutosha: mvua za kwanza na mvua za katikati kama pale mbele.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoeli 2:23
42 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

tafazali, uwasikilize kutokea kule mbinguni, usamehe zambi za watumishi wako, watu wako Waisraeli, na uwafundishe kufuata njia nzuri. Kisha unyeshe mvua katika inchi yako hii ambayo uliwapa watu wako kwamba itakuwa mali yao.


Lakini inawezekana kwamba malaika, ambaye ni mupatanishi mumoja kati ya maelfu, atakuwa karibu na mutu yule kwa kumufunulia jambo la kufanya.


Mungu anatimiza mapenzi yake katika dunia, ikuwe ni kwa ajili ya kuwaazibu watu, au kwa ajili ya kuonyesha wema wake.


Upendezwe na hayo mashairi yangu, ee Yawe, maana wewe ndiye furaha yangu.


Yeye anafunika anga kwa mawingu, anaitayarishia inchi mvua, na kuchipukiza nyasi kwenye vilima.


Umufurahie Muumba wako, ee Israeli; ninyi wakaaji wa Sayuni, mumushangilie mufalme wenu.


Yawe ndiye nguvu na ngao yangu; tegemeo la moyo wangu ni kwake. Amenisaidia, nami nikashangilia kwa moyo wote; kwa wimbo wangu ninamushukuru.


Mufurahi na kushangilia kwa sababu ya Yawe, enyi watu wa haki; mupige vigelegele vya shangwe, enyi wenye moyo wa usawa.


Heri watu wanaopata nguvu zao kwako, wanaotamani kusafiri kwa kuabudu kwa mulima wako.


Uso wa mufalme ukiangaa, kuna uzima; kupendwa naye ni kama wingu la mvua kwa shamba.


Mukienda kwa upande wa kuume au kushoto, mutasikia sauti nyuma yenu ikisema: Njia ni hii; muifuate.


Mutakapopanda mbegu zenu, Yawe atanyesha mvua kwa wakati wake, nazo zitakomaa na kuwapa mavuno mengi mazuri. Makundi yenu ya nyama nao watakula katika mashamba makubwa ya kukulishia nyama.


Mutaipepeta milima hiyo, nao upepo utaipeperushia mbali, zoruba itaitawanya huko na huko. Nanyi mutafurahi kwa sababu yangu Yawe; mutaona utukufu kwa sababu yangu Mungu Mutakatifu wa Israeli.


Nitafurahi sana kwa sababu ya Yawe, nafsi yangu itashangilia kwa sababu ya Mungu wangu. Maana amenivalisha nguo ya wokovu, amenifunika kanzu ya haki, kama bwana arusi anavyojipamba kwa shada la maua, kama bibi arusi anavyojipamba kwa ushanga wake.


Ndiyo maana manyunyu yamezuizwa kuanguka, wala mvua za mwisho hazijanyesha. Hata hivyo unakausha macho kama kahaba, wala hauna haya hata kidogo.


Wala hawasemi wenyewe hivi: Inatupasa kumwogopa Yawe, Mungu wetu, anayetujalia mvua kwa wakati wake, anayetupatia mvua za kwanza na mvua za mwisho; na kutupatia nyakati nzuri za mavuno.


Watoto wa Sayuni waliosifiwa sana, waliokuwa na bei kama zahabu safi, namna gani sasa wamekuwa kama vyombo vya udongo, kazi ya mikono ya mufinyanzi!


Nitawafanya waishi kandokando ya mulima wangu mutakatifu na kuwabariki. Nitawaletea mvua kwa wakati wake, nazo zitakuwa mvua za baraka.


Basi tumutambue, tujikaze sana kumujua Yawe. Kuja kwake ni hakika kama mapambazuko, yeye atatufikia kama vile manyunyu, kama vile mvua za kwanza zinavyolowanisha udongo.


nitawanyeshea mvua kwa wakati unaofaa, inchi ipate kuzaa mavuno kwa wingi, nayo miti ya mashamba matunda yake.


Tena niliwanyima mvua miezi mitatu tu mbele ya mavuno. Nilinyeshea mvua muji mumoja, na muji mwingine nikaunyima. Shamba moja lilipata mvua, na lingine halikupata, likakauka.


Muombe Yawe awape mvua za masika. Yawe ndiye anayeleta mawingu ya mvua; ndiye anayewapa watu mvua za manyunyu, na kustawisha mimea katika shamba kwa ajili ya wote.


Watu wa Efuraimu watakuwa kama mashujaa katika vita; watajaa furaha kama watu waliokunywa divai. Watoto wao wataona hayo na kufurahi, watajaa furaha ndani ya moyo kwa sababu yangu mimi Yawe.


Yuda nitamutumia kama upinde wangu; Efuraimu nimemufanya mushale wangu. Ee Sayuni, watu wako nitawatumia kama upanga kwa kuwashambulia watu wa Ugriki; watakuwa kama upanga wa shujaa.


Mushangilie sana enyi watu wa Sayuni! Mupige vigelegele, enyi watu wa Yerusalema! Angalia, mufalme wenu anawakujia, anakuja kwa shangwe na ushindi! Ni mupole, amepanda juu ya punda, juu ya mwana-punda, mutoto wa punda.


Ingawa vile hakuacha kujijulisha kwa njia ya kutenda mema. Anawanyeshea mvua toka mbingu, anawapa mavuno kwa wakati wake, anawapa chakula na kuwajaza na furaha.”


yeye ataipatia inchi yenu mvua wakati wake, mvua za kwanza na mvua za mwisho, nanyi mutavuna ngano yenu, divai yenu na mafuta yenu.


Yawe atawafungulia hazina yake nzuri kutoka mbinguni na kunyesha mvua katika inchi kwa wakati wake, na kubariki kazi zenu. Mutakopesha mataifa mengi, lakini ninyi hamutakopa.


Mafundisho yangu yatone kama mvua, maneno yangu yadondoke kama umande, kama manyunyu kwenye mimea michanga, kama mvua nyepesi katika majani mabichi.


Kwa kumaliza, wandugu zangu, mufurahi kwa ajili ya kuungana kwenu na Bwana. Hainiuzi kitu kuwaandikia tena maneno yale yale niliyowaandikia mbele. Hayo yote ni kwa ajili ya kuwakingia hatari.


Sisi ndio wenye kutahiriwa kwa kweli, maana tunamwabudu Mungu kwa uongozi wa Roho wake na kujivuna kwa ajili ya Yesu Kristo. Sisi hatuweki tumaini letu katika mambo ya kimwili.


Mufurahi siku zote katika kuungana kwenu na Bwana. Na tena ninasema: Mufurahi!


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ