Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoeli 2:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Muwakusanye watu wote, muwatakase watu. Muwalete wazee, muwakusanye watoto, hata watoto wanaonyonya. Bwana-arusi na bibi-arusi watoke katika vyumba vyao.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoeli 2:16
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wanaume wote wa Yuda, pamoja na wake zao na watoto wao, walikuwa wakisimama pale mbele ya Yawe.


akawaambia: “Munisikilize, enyi Walawi! Mujitakase na mutakase nyumba ya Yawe, Mungu wa babu zenu. Mutoshe uchafu wote unaokuwa katika Pahali Patakatifu.


Kwa vile ambavyo wengi wa wale waliokusanyika pale hawakukuwa wamejitakasa. Walawi walipaswa kuwachinjia wana-kondoo wa Pasaka na kuwatakasa kwa ajili ya Yawe.


atakayekuomba kwa moyo wake wote wewe Yawe, Mungu wa babu zake, hata ingawa yule mutu si musafi kulingana na sheria za utakaso.”


Muchinje mwana-kondoo wa Pasaka, mujitakase, halafu mutayarishe Pasaka kwa ajili ya wandugu zenu, kusudi waweze kutimiza neno la Yawe lililosemwa na Musa.”


Kila mara karamu ilipomalizika, Yobu aliita wana wake kusudi awatakase. Aliamuka asubui mapema kisha karamu, akatoa sadaka za kuteketezwa kwa moto kwa ajili ya kila mumoja wao maana aliwaza: “Labda wana wangu wametenda zambi na kumutukana Mungu ndani ya mioyo yao.”


hata hivyo, ujumbe wao unaenea katika dunia yote, na habari zao zinafika miisho ya ulimwengu. Mungu amewekea jua makao yake katika anga;


Yawe akamwambia Musa: “Kwenda kwa watu uwatakase leo na kesho. Uwaambie wafue nguo zao


Kisha akawaambia watu wote: “Kesho kutwa mukuwe tayari na mwanaume yeyote asimukaribie mwanamuke.”


Hata makuhani ambao wananikaribia wanapaswa kujitakasa, kama sivyo nitawaazibu.”


Mutoe amri watu wafunge kula chakula; muwaalike watu kuja kwa mukutano wa kidini. Mukusanye wazee na wakaaji wote wa inchi, katika nyumba ya Yawe, Mungu wenu, na mule mumulilie Yawe.


Basi wakamwuliza Yesu: “Unasikia maneno watoto hawa wanayoyasema?” Yesu akawajibu: “Ndiyo. Lakini hamujasoma Maandiko Matakatifu yanayosema: ‘Kwa vinywa vya watoto wadogo hata wale wanaokuwa wachanga umetangaza sifa zako.’ ”


Yesu akawajibu: “Munafikiri kwamba warafiki za bwana-arusi wanaweza kufanya kilio wakati bwana-arusi angali pamoja nao? Hapana! Lakini kutakuwa siku bwana-arusi atakapoondoshwa kati yao; ni siku zile watafunga kula.


Musinyimane, isipokuwa tu mumepatana na kwa muda tu kusudi mupate wakati wa kujitoa kwa kufunga na kuomba. Kisha munaweza kurudiliana tena kusudi Shetani asiwajaribu katika uzaifu wenu.


Basi, simama uwatakase watu, uwaambie wajitakase na kujitayarisha kwa siku ya kesho, maana mimi Yawe, Mungu wa Israeli, ninasema hivi: ‘Kati yenu kuna vitu vilivyotolewa viangamizwe. Hamuwezi kuwashinda waadui zenu mpaka vitu hivyo vimeondolewa kati yenu!


Hakuna neno lililoamriwa na Musa ambalo Yoshua hakulisoma mbele ya Waisraeli, kati yao kukiwa wanawake, watoto na wageni.


Samweli akawajibu: “Nimekuja kwa amani. Nimekuja kumutolea Yawe sadaka. Mujitakase wenyewe halafu tuende kutolea sadaka.” Samweli akamutakasa Yese pamoja na wana wake, akawakaribisha kwenye sadaka.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ