Wale nzige wakaenea kila pahali katika inchi ya Misri, wakatua juu ya inchi yote. Nzige wale walikuwa kundi kubwa sana, kiasi ambacho hakijapata kutokea wala hakitatokea tena.
Walifunika inchi yote ya Misri, hata inchi ikaonekana kuwa giza. Walikula mimea yote na matunda yote yaliyobaki wakati wa ile mvua ya mawe. Hakuna hata jani moja lililobakia katika inchi. Hakuna jani lolote lililobakia juu ya miti wala mimea popote katika inchi yote ya Misri.
Nitalifanya ukiwa kabisa, mizabibu yake haitasafishwa matawi wala kupaliliwa. Litaota michongoma na miiba. Tena nitayaamuru mawingu yasinyeshe mvua juu yake.
Nilitaka kuchuma matunda kutoka kwao. –Ni ujumbe wa Yawe.– Lakini sikupata zabibu hata moja juu ya muzabibu, sikupata tini zozote juu ya muti wa tini; hata majani yao yamekauka. Hata nilichokuwa nimewapa kimetoweka.
Niliwapiga pigo la ukosefu wa maji na ukungu; nikakausha bustani na mashamba yenu ya mizabibu; nzige wakakula miti ya tini na mizeituni yenu. Hata hivyo hamukunirudilia. –Ni ujumbe wa Yawe.–
Hata kama miti ya tini isipochanua maua wala mizabibu kuzaa zabibu, hata kama mizeituni isipozaa zeituni na mashamba yasipotoa chakula, hata kama kondoo wakitoweka katika zizi na nyama wa kufugwa kukosekana katika mazizi,