Kama muti wa matunda kati ya miti ya pori, ndivyo mupenzi wangu anavyokuwa kati ya vijana. Ninafurahia kuikaa chini ya kivuli chake, na tunda lake tamu sana kwangu.
Furaha na shangwe zimetoweka katika shamba lenyi mavuno mengi. Kwenye mizabibu hakuna kuimba tena, wala kupiga vigelegele. Hakuna tena kukamua zabibu ndani ya vikamulio, sauti za furaha za mavuno zimekomeshwa.
Furaha na shangwe zimeondolewa kutoka inchi ya Moabu yenye mboleo. Nimeikomesha divai kutoka katika vikamulio. Hakuna mutu anayekamua mizabibu kwa shangwe; kelele zinazosikilika si za shangwe.
Walipofika katika Bonde la Eskoli, watu hao wakakata shada la muzabibu lililokuwa na matunda mengi nalo lilibebwa na watu wawili juu ya muti. Wakatwaa vilevile makomamanga na tini.