Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yobu 9:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Yeye anahamisha milima bila yenyewe kutambua, anaipindua mbali kwa hasira yake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yobu 9:5
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kuzimu kuko wazi kabisa mbele ya Mungu. Shimo la kuangamia halina kifuniko chochote.


Mwanadamu anachimbua mawe magumu kabisa, anachimbua milima mpaka kwenye misingi yake.


Kwa maana anayajua matendo yao yote, anawapindua usiku waangamie.


Uwamwangie watu hasira yako kubwa; umwangalie kila mwenye kiburi na kumwangusha.


Katika kinywa chake kunatokea mienge inayowaka, cheche za moto zinaruka inje.


Enyi milima, mbona muliruka kama kondoo dume? Nanyi vilima, namna gani mumeruka kama mwana-kondoo?


Mungu ni kimbilio letu na nguvu yetu; yeye ni musaada wetu wakati wa taabu.


Ee Mungu, ulipowaongoza watu wako, uliposafiri kule katika jangwa,


Ni nani anayeweza kupima maji ya bahari katika kitanga cha mukono wake, na kuzipima mbingu kwa mikono yake? Ni nani anayeweza kuutia udongo wa dunia katika kikombe; kuipima milima kwa mizani au vilima kwa kipimo cha uzito?


Milima inatetemeka mbele yake, vilima vinayeyuka. Dunia inatetemeka mbele yake, ulimwengu na vyote vinavyokuwa ndani yake.


Nani anayeweza kusimama mbele ya kasirani ya Yawe? Nani anayeweza kuvumilia ukali wa hasira yake? Yeye anaimwanga hasira yake inayowaka kama moto, hata mawe makubwa anayapasua vipandevipande.


Milima ilikuona, ikanyauka; mafuriko ya maji yakapita mule. Vilindi vya bahari vilinguruma, na kurusha juu mawimbi yake.


Akisimama dunia inatikisika; akiyatupia mataifa jicho, hayo yanatetemeka. Milima ya milele inavunjwavunjwa, vilima vya zamani za kale vinaanguka; ni juu yao kulipokuwa njia zake za kale na kale.


Tena, akaongeza kusema: Mulima huu ni kizuizi? Hapana! Wewe Zerubabeli utausawazisha. Wewe utaanzisha ujenzi mupya wa hekalu, na wakati utakapoliweka jiwe la mwisho, watu watashangilia wakisema: Ni zuri! Kweli, ni zuri!


Yesu akawajibu: “Kweli ninawaambia: mukimwamini Mungu pasipo kuwa na shaka, hamutaweza kufanya tu kama nilivyotendea muti huu, lakini vilevile mutaweza kuuambia mulima huu: ‘Ondoka hapa, ujitupe katika bahari,’ na itakuwa vile.


Na saa ile ile pazia la hekalu likapasuka vipande viwili toka juu mpaka chini. Inchi ikatetemeka, mawe makubwa yakapasuka,


Kutakuwa tetemeko kubwa la inchi. Vilevile kutakuwa njaa na magonjwa makali kwenye nafasi mbalimbali. Zaidi ya ile kutakuwa mambo ya kuogopesha na vitambulisho vya ajabu toka mbinguni.


Hata nikiwa na zawadi ya kutabiri, na uwezo wa kujua mafumbo yote na maarifa yote; hata nikiwa na imani kubwa inayoweza kuhamisha milima; lakini kama sina upendo, mimi ni kitu bure.


Na saa ile ile, kukatokea tetemeko kubwa la inchi, na sehemu moja ya kumi ya muji ikabomoka, na watu elfu saba wakakufa katika tetemeko lile. Watu waliobaki wakashikwa na hofu, nao wakamutukuza Mungu wa mbinguni.


Mbingu zikaviringwa na kuwa kama kizingo cha karatasi na kutoweka. Milima yote na visanga vyote vikahamishwa kutoka kwenye nafasi yao.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ