Na muangalie, Mungu mwenyewe ndiye kiongozi wetu na makuhani wake wako na baragumu zao tayari kuzipiga kwa kupana kitambulisho cha kuanza vita juu yenu. Enyi watu wa Israeli, muache kupigana vita na Yawe, Mungu wa babu zenu. Hamuwezi kushinda!”
akaomba kwa sauti akisema: “Ee Yawe, Mungu wa babu zetu, wewe ndiwe Mungu unayekuwa mbinguni! Wewe unatawala falme zote katika dunia, una uwezo na nguvu, wala hakuna anayeweza kukupinga.
Mufalme wa Misri akauliza habari juu ya nyama wa Waisraeli. Wakamwambia kwamba hakuna nyama wao hata mumoja aliyekufa. Hata hivyo, Mufalme akabaki akifanya moyo wake kuwa mugumu, wala hakuwaruhusu Waisraeli waondoke.
Ole kwake mutu anayebishana na Muumba wake: chombo cha udongo kubishana na mufinyanzi wake! Udongo unamwuliza anayeufinyanga: Unatengeneza nini hapa? au kumwambia: Kazi yako si kamili!
Yawe hakasiriki upesi, lakini amejaa nguvu, Yawe hatawaachilia wenye makosa hata kidogo. Yawe anapopita, upepo mukali na zoruba vinatokea; mawingu ni mavumbi yanayonyanyuliwa na miguu yake.
Lakini sasa, kwa njia ya kanisa, watawala na wote wenye uwezo wanaokuwa katika eneo la mbingu wapate kutambua hekima ya Mungu inayokuwa ya namna nyingi.