Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yobu 9:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Yeye ni mwenye hekima sana na nguvu nyingi. Nani aliyepingana naye, akashinda?

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yobu 9:4
39 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Na muangalie, Mungu mwenyewe ndiye kiongozi wetu na makuhani wake wako na baragumu zao tayari kuzipiga kwa kupana kitambulisho cha kuanza vita juu yenu. Enyi watu wa Israeli, muache kupigana vita na Yawe, Mungu wa babu zenu. Hamuwezi kushinda!”


akaomba kwa sauti akisema: “Ee Yawe, Mungu wa babu zetu, wewe ndiwe Mungu unayekuwa mbinguni! Wewe unatawala falme zote katika dunia, una uwezo na nguvu, wala hakuna anayeweza kukupinga.


Angekuelezea siri za hekima, maana yeye yuko na maarifa mengi. Ujue kwamba Mungu hakuhesabu makosa yako yote.


Lakini hekima na uwezo ni vya Mungu. Yeye ana maarifa na ujuzi.


hata kumwasi Mungu na kusema maneno mabaya kama yale?


Angeshindana nami kwa nguvu zake zote? Hapana! Bila shaka angenisikiliza.


Mungu, kwa nguvu yake, anawaangamiza wenye uwezo; anasimama, nao wanakata tamaa ya kuishi.


Mungu ni mwenye uwezo mukubwa, watu wote wamwogope. Yeye anaweka amani mpaka juu kwake mbinguni.


Mungu anajua njia ya hekima, anajua pahali inapopatikana.


Sikia! Mungu ni mwenye nguvu wala hamuzarau mutu yeyote; uwezo wa akili yake ni mukubwa sana!


Mungu Mwenye Uwezo asiyeweza kufikiwa na mutu, uwezo na haki yake ni mukubwa. Amejaa haki wala hapotoshi sheria hata kidogo.


Ni nani aliyemujulisha kwarara kujaa kwa muto Nili au aliyemwambia jogoo kwamba mvua inakuja?


Nani mwenye akili ya kuweza kuhesabu mawingu au kuinamisha vibuyu vya maji kule katika mbingu


Una nguvu kama mimi Mungu? Unaweza kunguruma kwa sauti kama yangu?


Hakuna mutu yeyote mukali anayesubutu kumushitua. Nani, basi anayeweza kusimama mbele yangu?


Hiyo ingekuwa faraja yangu, ningefurahi katika maumivu yasiyokuwa na huruma, kwa sababu sikukataa maagizo ya Mungu Mutakatifu.


Kama ni kushindana, yeye ana nguvu sana! Na kama ni kutafuta juu ya haki, nani atakayemuleta mbele ya tribinali?


Ee Yawe, matendo yako ni mengi sana! Umeyafanya kwa hekima yote! Dunia imejaa viumbe vyako!


Aliumba mbingu kwa hekima. Wema wake unadumu milele.


Kwa wingi wa ukubwa wako unawaangamiza wapinzani wako; unawapulizia kasirani yako nayo inawateketeza kama maganda.


Mufalme wa Misri akauliza habari juu ya nyama wa Waisraeli. Wakamwambia kwamba hakuna nyama wao hata mumoja aliyekufa. Hata hivyo, Mufalme akabaki akifanya moyo wake kuwa mugumu, wala hakuwaruhusu Waisraeli waondoke.


Heri mutu anayemwogopa Yawe siku zote, lakini mwenye moyo mugumu atapata hasara.


Anayeonywa mara nyingi na kuwa mugumu, ataangamia kwa rafla wala hatapata kupona.


Ole kwake mutu anayebishana na Muumba wake: chombo cha udongo kubishana na mufinyanzi wake! Udongo unamwuliza anayeufinyanga: Unatengeneza nini hapa? au kumwambia: Kazi yako si kamili!


Ewe Babeli, nilikutegea mutego ukanaswa, wala haukujua kitu juu yake; ulipatikana, ukakamatwa, kwa sababu ulishindana nami Yawe.


akasema: Jina la Mungu litukuzwe milele na milele. Hekima na nguvu ni vyake.


Yawe hakasiriki upesi, lakini amejaa nguvu, Yawe hatawaachilia wenye makosa hata kidogo. Yawe anapopita, upepo mukali na zoruba vinatokea; mawingu ni mavumbi yanayonyanyuliwa na miguu yake.


Utajiri wa Mungu, hekima na ufahamu wake ni vikubwa kupita kipimo! Hakuna anayeweza kuvumbua kusudi lake wala kuelewa mipango yake!


Au tunataka kumuchokoza Bwana hata asikie wivu? Munafikiri kuwa sisi tuko na nguvu kuliko yeye?


na kutambua jinsi uwezo wake unavyokuwa mukubwa sana kwa ajili yetu sisi waamini, akizitumia nguvu zake kubwa sana.


Lakini sasa, kwa njia ya kanisa, watawala na wote wenye uwezo wanaokuwa katika eneo la mbingu wapate kutambua hekima ya Mungu inayokuwa ya namna nyingi.


Basi, Mungu ambaye kwa nguvu yake inayofanya kazi ndani yetu, anaweza kufanya mambo makubwa zaidi yanayopita yale tunayoweza kuomba au kufikiri;


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ