3 Kama mutu angesubutu kushindana naye, hataweza kufika mbali, hata kujibu ulizo moja kati ya elfu.
Nitamwambia Mungu: Usinitendee sawa na mwenye makosa. Unijulishe sababu ya kugombana nami.
Nani atakayebishana nami? Niko tayari kunyamaza na kufa.
Kwa nini unashindana naye, ukisema hatajibu ulizo lako moja?
Mungu hahitaji kumujulisha mutu wakati wa kumuleta mbele ya tribinali yake.
Wewe mwenye kuchunguza makosa utashindana na Mungu Mwenye Uwezo? Wewe unayebishana nami Mungu, basi ujibu mambo hayo!
Nilisubutu kusema na sitasema tena. Nilisema mengi lakini sitaendelea kusema zaidi.
Nitaweza namna gani basi kumujibu Mungu? Nitachagua wapi maneno ya kumwambia?
Ingawa sina kosa, maneno yangu yenyewe yangenihukumu. Ingawa mimi ni mukamilifu, yangehakikisha kwamba mimi ni mupotovu.
Yananifundisha mimi mutumishi wako; kuyafuata kunaniletea zawadi kubwa.
Ee Yawe, usikose kunirehemu! Wema na uaminifu wako vinilinde.
Halafu sasa wewe mwanadamu ni nani hata ubishane na Mungu? Chombo cha udongo hakiwezi kumwuliza mufinyanzi: “Kwa nini umenitengeneza hivi?”
Tukisema kwamba hatuna zambi, tunajidanganya sisi wenyewe, wala ukweli hauko ndani yetu.
Kwa maana hata kama zamiri yetu inatuhukumu, tunajua kwamba mafikiri ya Mungu yanapita zamiri yetu, naye anajua yote.