Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yobu 9:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Kweli ninajua kama ni hivi. Lakini mutu anaweza namna gani kuwa haki mbele ya Mungu?

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yobu 9:2
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

“Ikiwa watatenda zambi mbele yako, maana hakuna mutu asiyetenda zambi, nawe ukiwakasirikia na kuwaacha washindwe na adui, hata wapelekwe mateka mpaka katika inchi ya adui inayokuwa mbali au karibu,


Ee Yawe, Mungu wa Israeli, wewe ni mwenye haki na umetuacha tubaki kama vile tunavyokuwa hivi leo. Tunaungama makosa yetu mbele yako, tukijua kwamba hakuna anayekuwa na haki yoyote ya kuja mbele yako kwa ajili ya makosa haya.”


Mutu anaweza basi namna gani kuwa mwenye haki mbele ya Mungu? Mwanadamu tu anaweza namna gani kujidai kuwa safi?


Kwake Mungu, hata mwezi hauangai vya kutosha, nyota nazo si safi mbele yake;


Kwa hiyo Elihu mwana wa Barakeli wa kabila la Buzi wa ukoo wa Rama akakasirika. Alimukasirikia Yobu kwa sababu Yobu alijiona yeye mwenye haki na wala si Mungu.


Wewe umesema hivi: “Mimi niko safi, wala sina kosa. Hakuna ubaya wowote katika moyo wangu.


Basi, Yobu amesema: “Mimi Yobu sina kosa, Mungu ameniondolea haki yangu.


“Mwanadamu anaweza kuwa mwenye haki mbele ya Mungu? Mutu anaweza kuwa safi mbele ya Muumba wake?


Ee Yawe, kama ungekumbuka maovu yetu, nani, ee Bwana wetu, angeweza kuishi?


Usinitie katika hukumu mimi mutumishi wako, maana hakuna yeyote anayekuwa mwenye haki mbele yako.


Kwa sababu hakuna mutu atakayehesabiwa haki mbele ya Mungu kwa kuwa anatii Sheria, maana Sheria inamusaidia mutu tu kwa kutambua kwamba amefanya zambi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ