Nyuma, Rehoboamu akataka kujua maoni ya wazee ambao walikuwa washauri wa baba yake Solomono alipokuwa angali muzima, akawauliza: “Munanishauria kwamba niwape jibu gani watu hawa?”
Musikilize kitu hiki, enyi wazee; mutege sikio, ninyi wakaaji wote wa Yuda! Jambo kama hili limekwisha kutokea katika maisha yenu, au nyakati za babu zenu?
Na yote yaliyoandikwa zamani katika Maandiko Matakatifu yameandikwa kwa ajili ya kutufundisha sisi, kusudi tuendelee kuchunga tumaini kwa njia ya kuvumilia na kufarijiwa sawa tunavyofundishwa katika Maandiko Matakatifu.
Mambo haya yote yaliwafikia kusudi yakuwe mufano kwa watu wengine; yameandikwa kwa kutuonya sisi, kwa maana tunaishi katika kipindi cha mwisho wa nyakati.
“Mufikiri sana juu ya matukio ya zamani, mambo yaliyotukia mbele ninyi hamujazaliwa, tangu siku ile Mungu alipomwumba mutu katika dunia. Muulize katika ulimwengu wote, toka pembe moja mpaka nyingine, kama jambo la ajabu la namna hii limepata kutokea au kusikilika!