Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yobu 8:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Ndivyo wote wanaomusahau Mungu wanavyokuwa. Tumaini la wasiomwamini Mungu litapotea.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yobu 8:13
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini waovu macho yao yatafifia, njia zote za kutorokea zitawapotea; tumaini lao la mwisho ni kukata roho!


Kama nikiweza kwa hiyo nitakuwa nimeshinda, maana mutu mwovu hawezi kwenda mbele yake.


Wote wasiomwogopa Mungu hawatapata watoto, moto utateketeza mahema ya wanaokula kituliro.


Anaongolewa katika nyumba aliyotegemea, na kupelekwa kwa mufalme wa vitisho.


mwovu atajiona ameshinda kwa muda tu, furaha ya asiyemwogopa Mungu ni ya muda mufupi tu!


Waovu wanapenda kukasirika; hawamwombi musaada anapowafunga.


Hata kama yamechanua na bila kukatwa, yakikosa maji yananyauka mbele ya mimea mingine.


Lakini waovu si vile hata kidogo. Wao ni kama maganda yanayopeperushwa na upepo.


Katika majivuno yake anasema: “Mungu hatagundua. Hakuna Mungu.” Hayo ndiyo mawazo yake yote.


Watu waovu wanaona hayo na kuuzika. Wanasaga meno kwa chuki na kutoweka. Matumaini ya mutu mubaya yanapotea bure.


“Mufikiri vizuri jambo hili, enyi musionijali, kama sivyo nitawaangamiza, wala hakuna atakayewaokoa.


Yawe amejitambulisha; anatoa hukumu. Waovu wamenaswa kwa matendo yao wenyewe.


Tumaini la mwenye haki linaleta furaha, lakini tazamio la mwovu linapotea bure.


Mwovu akikufa, tumaini lake nalo linatoweka. Tumaini la asiyemwogopa Mungu ni la bure.


Waovu wanaangamizwa na kutoweka kabisa, lakini jamaa ya wenye haki itasimama.


Wenye zambi katika Sayuni wanaogopa, wasiomwamini Mungu wanatetemeka na kusema: Nani anayeweza kuvumilia moto huu mukali? Nani anayeweza kuvumilia ndimi za moto usiozimika?


Wewe umenisahau mimi Yawe Muumba wako, niliyezitandaza mbingu, na kuiweka misingi ya dunia! Kwa sababu ya kasirani ya yule anayekutesa, unaendelea kuogopa siku zote kwamba yuko tayari kukuangamiza! Lakini hasira yake itafikia wapi?


Nimewaza: Nimekata tamaa kabisa, tumaini langu kwa Yawe limetoweka.


Naye atamupiga vikali na atamwazibu sawa na watu wanafiki, akimuweka kwenye nafasi atakapolia na kusaga meno.


muhakikishe kwamba hamutamusahau Yawe aliyewatoa Misri ambako mulikuwa watumwa.


“Muhakikishe kwamba hamutamusahau Yawe, Mungu wenu, kwa kutoshika amri zake, maagizo yake na masharti yake ninayowaamuru leo.


musikuwe na kiburi na kumusahau Yawe, Mungu wenu, aliyewatoa katika inchi ya Misri, pahali mulipokuwa watumwa.


Lakini mukimusahau Yawe, Mungu wenu, na kufuata miungu mingine kwa kuitumikia na kuiabudu, ninawaonya vikali leo hii kwamba hakika mutaangamia.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ