12 Hata kama yamechanua na bila kukatwa, yakikosa maji yananyauka mbele ya mimea mingine.
mwovu atajiona ameshinda kwa muda tu, furaha ya asiyemwogopa Mungu ni ya muda mufupi tu!
Nyasi zinaota tu penye tingitingi, matete yanastawi pahali panapokuwa maji.
Ndivyo wote wanaomusahau Mungu wanavyokuwa. Tumaini la wasiomwamini Mungu litapotea.
Mifereji yake itatoa harufu mbaya, vijito vyake vitapunguka na kukauka. Nyasi na matete yake yataoza.
Huyo ni kama kichaka katika jangwa, hataona mazuri yoyote. Ataishi pahali penye kukauka katika jangwa, kwenye udongo ulioharibiwa na chumvi, na usiokaliwa na watu.
Udongo wenye mawe pahali mbegu zilipoanguka ni mufano wa watu wanaosikia Neno la Mungu, na mara moja wanalipokea kwa furaha.
Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Wanadamu wote ni kama majani. Na utukufu wao wote unatoweka kama maua. Majani yanakauka na maua yanaanguka.