4 Ninapolala ninasema: “Nitaamuka wakati gani?” Maana saa za usiku ni ndefu sana; ninagaagaa katika kitanda mpaka mapambazuko!
Kwa hao watu, usiku ni muchana: wanasema kwamba mwangaza unakaribia giza.
Usiku mifupa yangu yote inauma; maumivu yanayonitafuna hayapoi.
Ninatoweka kama kivuli cha magaribi; nimepeperushwa kama nzige.
Ninamungojea Yawe kuliko vile wazamu wanavyongojea mapambazuko, ndiyo, kuliko vile wazamu wanavyongojea mapambazuko.
Huko kwa wafu hakuna anayekukumbuka; katika kuzimu ni nani anayeweza kukusifu?
Ninafikiri juu ya Mungu na kuugua; ninamukumbuka na kufa moyo.
Ewe Yerusalema, uliteseka, ulitaabishwa na kukosa wa kukufariji, lakini nitakujenga upya kwa mawe ya bei kali, misingi yako itakuwa ya mawe ya yakuti.
Mioyo yenu itajaa woga wa kila kitu mutakachoona. Asubui mutasema ‘Heri ingekuwa magaribi’; magaribi itakapofika mutasema ‘Heri ingekuwa asubui’.