3 Basi nimepangiwa miezi na miezi ya taabu, urizi wangu ni kuteseka usiku kwa usiku.
Kweli Mungu amenichakalisha, ameharibu kila kitu karibu nami.
Anatimiza yote aliyonipangia; na mengi kama hayo yako katika akili yake.
Heri ningekuwa kama zamani, wakati ule ambapo Mungu alinichunga,
Yeye ni kama mutumwa anayetamani kivuli, kama mutumishi anayengoja kwa hamu mushahara wake.
“Ee Yawe, unijulishe mwisho wangu, siku zangu za kuishi zimenibakia ngapi, nijue namna maisha yangu yanavyopita upesi!”
Huko kwa wafu hakuna anayekukumbuka; katika kuzimu ni nani anayeweza kukusifu?
Ninatabanika kwa kulia kwa uchungu; usiku ninalowanisha kitanda changu kwa machozi; kwa kulia kwangu ninalowanisha matandiko yangu.
Nimeyaona mambo yote yanayofanywa chini ya jua. Yote ni bure sawa na kutaka kukamata upepo!