Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yobu 7:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Yeye ni kama mutumwa anayetamani kivuli, kama mutumishi anayengoja kwa hamu mushahara wake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yobu 7:2
11 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini Hamori akawaambia: “Mwana wangu Sekemu anamupenda sana binti yenu. Basi, tafazali mumuruhusu amwoe.


Mwanadamu ana magumu katika dunia, na siku zake ni kama siku za mutumishi wa mushahara!


Basi nimepangiwa miezi na miezi ya taabu, urizi wangu ni kuteseka usiku kwa usiku.


Ninafungua kinywa kwa hamu kubwa, maana ninatamani sana amri zako.


Ninakunyooshea mikono yangu. Ninakuhitaji wewe, kama inchi kavu inavyohitaji mvua.


Halafu watasema: Mujitayarishe, tupigane vita na Sayuni. Musimame, tuushambulie pa saa sita za muchana! Bahati mbaya kwetu, maana jua linatua! Saa za magaribi zinakaribia.


Usimutese mwenzako wala kumwibia. Usikae na mushahara wa mutumishi wako usiku kucha mpaka asubui.


Mungu, Yawe akaamuru mumea uote na kukomaa. Akauotesha kwa kumupatia Yona kivuli cha kumupunguzia taabu aliyokuwa nayo. Yona akaufurahia sana mumea huo.


Yawe wa majeshi anasema: Kisha nitawakaribia kwa kuwahukumu. Sitasita kutoa ushuhuda juu ya wachawi, wazinzi, watoa ushuhuda wa uongo, wanaopunja mushahara wa watumishi, wanaowatesa wajane na wayatima, wanaozuia mugeni asipate haki yake na wale wasioniogopa mimi.


Kila siku, mbele jua halijatua, umulipe mushahara wake wa siku hiyo, maana yeye ni masikini na huo mushahara ni tegemeo la moyo wake; kusudi asimulilie Yawe, nawe utakuwa na kosa.


Ninyi hamukulipa mishahara ya watumishi waliotumika katika mashamba yenu. Musikilize mashitaki yao! Malalamiko ya wavunaji yamefika katika masikio ya Bwana Mwenye Uwezo!


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ