Hakuna mutu anayekuwa na uwezo wa kushikilia roho yake kusudi asikufe; hakuna mutu anayekuwa na uwezo juu ya siku ya kufa. Wakati wa vita hakuna kuponyoka, na uovu hauwezi kumwokoa mwovu.
Lakini sasa Yawe anasema hivi: Nyuma ya miaka mitatu kamili, ikihesabiwa kama vile mutumishi anavyohesabu siku zake, utukufu wa Moabu utapunguka. Ingawa watu wake ni wengi, watakaobaki wazima watakuwa wachache na wazaifu.
Kwenda umwambie Hezekia kwamba: Mungu wa baba yako Daudi, anasema hivi: Nimesikia ombi lako na nimeyaona machozi yako. Basi, ninakuongezea miaka kumi na mitano ya kuishi.
Museme na watu wa Yerusalema kwa upole, muwaambie kwamba utumwa wao umekwisha, wamesamehewa uovu wao. Yawe amewaazibu mara mbili kwa sababu ya zambi zao zote.
Yeye akishirikiana na yule aliyemununua, atahesabu miaka tangu alipojiuzisha mpaka mwaka wa kukumbuka miaka makumi tano. Malipo ya kuachiliwa huru kwake italingana na miaka aliyomutumikia. Muda ambao amekuwa mutumwa wa bwana wake utapimwa kama muda wa mutumishi wa kulipiwa.
Wala usione ugumu utakapomwacha huru mutumwa wako, maana, amekutumikia kwa muda wa miaka sita kwa nusu ya mushahara wa mutumishi wa kulipwa. Fanya hivyo, naye Yawe, Mungu wako, atakubariki kwa kila utakalofanya.