Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yobu 5:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Mazao yake yanakuliwa na wenye njaa, hata ngano iliyoota kati ya miiba. Wenye tamaa wananyanganya utajiri wake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yobu 5:5
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa hiyo, Yawe akawaleta majemadari wa jeshi la mufalme wa Asuria. Hao majemadari wakamukamata Manase kwa ndoana, wakamufunga kikomo cha shaba, wakamupeleka mpaka Babeli.


Basi Wasabea wakatushambulia na kunyanganya nyama na kuua watumishi kwa upanga. Ni mimi tu peke yangu nimepona kwa kuja kukuletea habari.”


Yule naye alipokuwa hajamaliza kusema, mwingine akafika, akasema: “Wakaldea walijipanga makundi matatu, wakashambulia ngamia, wakawatwaa, na wakaua watumishi wako kwa upanga! Ni mimi tu peke yangu nimepona kwa kuja kukuletea habari.”


Makao ya wanyanganyi yana amani. Wenye kumuchokoza Mungu wako salama; nguvu yao ni mungu wao.


Yawe akamwambia Shetani: “Umemwona vizuri mutumishi wangu Yobu? Katika dunia hakuna mwingine anayekuwa kama yeye. Yeye ni mutu mukamilifu, wa usawa, mwenye kumwogopa Mungu na mwenye kuepukana na uovu. Yeye anadumu katika ukamilifu, ingawa wewe umenisukuma nimwangamize bure.”


Mwovu anameza mali haramu na kuitapika; Mungu anaitoa ndani ya tumbo lake.


Atakapotajirika sana atapatwa na taabu, hasara itamupata kwa nguvu zote.


Kwa hiyo mitego imekuzunguka pande zote, hofu ya rafla imekupata.


Anayemudai kitu amunyanganye mali yake yote, na wageni wakule mapato ya jasho lake!


Yawe ameapa kwa uwezo wake mukubwa, ameapa kwa nguvu yake akisema: Sitawapa tena waadui zako ngano yako; wala wageni hawatakunywa tena divai yako ambayo umeitoshea jasho.


Mufalme Nebukadneza wa Babeli aliuharibu na kuuponda Yerusalema aliuacha kama chungu kitupu; aliumeza kama vile nyoka mukubwa. Alijaza tumbo lake vitu vyake vizurivizuri, akautupilia mbali kama matapiko.


Nitamwazibu mungu Beli huko Babeli, nitamutapikisha kile alichomeza. Mataifa hayatamwendea tena kwa wingi. Ukuta wa Babeli umebomoka.


Waadui zako wote wanakuzomea, wanakupigia muunzi na kukusagia meno, nao wanasema: Tumemwangamiza! Kweli, siku ile tuliyoingojea kwa hamu sasa imefika na tumeiona!


Yawe amekuwa kama adui, ameangamiza watu wa Israeli; ameharibu nyumba zake kubwa zote, amevibomoa vikingio vyake. Amewazidishia watu wa Yuda kilio na maombolezo.


Wanapanda upepo, watavuna zoruba! Mimea yao ya ngano inayokuwa katika mashamba haitatoa ngano yoyote. Na hata kama ikizaa, mazao yake yatakuliwa na wageni.


“Taifa musilolijua litatwaa mazao yote ya inchi yenu na matunda ya jasho lenu, nanyi mutapondwa na kuteswa siku zote,


Watakula ngombe wenu na mazao yenu, mpaka muangamie. Hawatawaachia ngano, divai, mafuta, ngombe au kondoo mpaka wawaangamize.


Malaika wa Yawe akaenda, akaikaa chini ya muti wa mwalo wa Yoasi Mwabiezeri, kule Ofura. Gideoni mwana wa Yoasi alikuwa anapepeta ngano ndani ya kikamulio cha kukamulia zabibu kusudi Wamidiani wasimwone.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ