26 Utashuka katika kaburi ukiwa na miaka yenye kutimia, kama vile muganda wa ngano uliokomaa vizuri.
Lakini wewe mwenyewe utaishi maisha marefu na kufa kwa amani.
Kisha kuishi maisha marefu na ya fanaka, akakufa na kukutana na wazee wake.
Basi haya ndiyo mambo tuliyochunguza. Ni hivi tu. Uyasikie na kuyaelewa kwa faida yako.
Nitamupa maisha marefu, nitamujalia wokovu wangu.”
Hakutakuwa mwanamuke yeyote atakayepoteza mimba wala kuwa tasa katika inchi yenu. Nami nitawajalia maisha marefu.
Kumwogopa Yawe kunarefusha maisha, lakini miaka ya waovu itakuwa mifupi.
Kwa musaada wangu mimi Hekima siku zako zitaongezwa; utaongezewa miaka mingi katika maisha yako.
Hakutakuwa tena vifo vya watoto wachanga, wazee nao hawatakufa mbele ya wakati wao. Mutu wa miaka mia moja akikufa, amekufa akiwa kijana; na akikufa mbele ya miaka mia moja, ni kusema amelaaniwa.
Musa alikuwa na umri wa miaka mia moja na makumi mbili alipokufa. Macho yake yalikuwa hayajafifia, na nguvu za mwili wake hazikupunguka.