Imbwa wa pori na kondoo watakula pamoja, simba watakula majani kama ngombe, lakini chakula cha nyoka kitakuwa mavumbi. Katika mulima wangu wote mutakatifu, hakuna atakayeumiza au kuharibu kitu. –Ni Yawe anayesema hivyo.
Miti inayokuwa katika mashamba itazaa matunda, udongo utatoa mazao kwa wingi, nao wataishi kwa salama katika inchi yao. Nitakapovunja nira zao za utumwa na kuwaokoa toka katika mikono ya hao waliowafanya kuwa watumwa halafu watatambua kwamba mimi ni Yawe.