Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yobu 5:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Anawanasa wenye hekima kwa werevu wao, anakomesha mara moja mipango ya waovu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yobu 5:13
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakati ule, Daudi aliambiwa kwamba hata Ahitofeli alikuwa mumoja wa waasi waliojiunga na Abusaloma. Lakini Daudi akaomba akisema: “Ee Yawe, ninakuomba uyafanye mashauri ya Ahitofeli yasifanikiwe.”


Urudi Yerusalema na kumwambia Abusaloma: ‘Nitakuwa mutumishi wako, ee mufalme, kama vile nilivyokuwa zamani mutumishi wa baba yako’. Kwa njia hiyo utanisaidia kupinga mashauri ya Ahitofeli.


Ahitofeli alipoona kwamba shauri lake halikufuatwa, alitandika punda wake, akaenda kwake, kwenye muji wake. Alipofika kule, alipanga vizuri mambo ya nyumba yake, akajitundika. Akakufa na kuzikwa kwenye kaburi la baba yake.


Naye, Hamani akauawa pale kwenye muti aliokuwa amemutayarishia Mordekayi. Basi, hasira ya mufalme ikapoa.


Lakini Esteri alipomwendea mufalme, naye mufalme akatoa amri kwa waandishi kwamba lile shauri baya ambalo Hamani alikuwa amefanya juu ya Wayuda, limurudilie yeye mwenyewe; na ya kuwa yeye na wana wake wauawe kwa kutundikwa kwenye muti.


Uovu wako ndio unaongoza kinywa chako, nawe unachagua kusema kama wadanganyifu.


Kwa hiyo, watu wote wanamwogopa. Yeye hawajali watu wanaojiona kuwa wenye hekima.


Wewe ni mwema kwa wema, mukamilifu kwa wakamilifu,


Yawe amejitambulisha; anatoa hukumu. Waovu wamenaswa kwa matendo yao wenyewe.


Maana waovu ni chukizo kwa Yawe, yeye anawafanya watu wa usawa kuwa warafiki zake.


Nitawaondolea Wamisri uhodari wao. Nitaivuruga mipango yao. Watatafuta shauri kwa sanamu na mizimu, wachawi, mizuka na pepo.


Mimi ninavuruga maono ya manabii wa uongo na ninapoteza akili za waaguzi. Mimi ninayapinga maneno ya wenye hekima na kufanya elimu yao kuwa upumbafu.


Kisha, watu wakasema: Tuende tufanye shauri baya juu ya Yeremia, maana hatukosi makuhani wa kutufundisha. Vilevile hatukosi watu wenye hekima wa kutushauria na manabii wa kututangazia ujumbe wa Mungu! Mukuje tumushitaki kufuatana na maneno yake mwenyewe, wala tusiyatilie maana mambo yote anayosema.


Juu ya Edomu, Yawe wa majeshi anasema hivi: Hakuna tena hekima katika muji wa Temani? Wenye hekima wao hawana shauri tena? Hekima imetoweka kabisa?


Ninyi munajidai kwamba muko na hekima, nanyi munafuata amri zangu mimi Yawe. Lakini kalamu ya uongo ya waandishi imeifanya kuwa uongo.


Wenye hekima kati yenu wanafezeheka, watahangaishwa na kunaswa. Wamelikataa neno la Yawe. Basi ni hekima gani wanayokuwa nayo?


Yawe anasema hivi: Mwenye hekima asijivunie hekima yake, mwenye nguvu asijivunie nguvu yake; wala tajiri asijivunie utajiri wake.


Punda alipomwona malaika huyo wa Yawe, akajibanisha kwenye ukuta na kubana muguu wa Balamu hapo. Kwa hiyo Balamu akamupiga tena huyo punda.


Ametenda kwa uwezo wake mukubwa, amewasambaza wale wanaofanya mipango kwa kiburi.


Kwa maana hekima ya kidunia ni upumbafu mbele ya Mungu. Ni sawa vile Maandiko Matakatifu yanavyosema: “Mungu anawanasa wenye hekima katika werevu wao wenyewe.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ