Abusaloma pamoja na watu wote wa Israeli wakasema: “Shauri la Husayi ni bora kuliko shauri la Ahitofeli.” Wakakataa shauri la Ahitofeli kwa sababu Yawe alikuwa amepanga kulishinda shauri jema la Ahitofeli kusudi aweze kumuletea Abusaloma hasara.
Waadui waliposikia kwamba tumekwisha kuvumbua mipango yao na kwamba Mungu amevuruga mipango hiyo, ndipo sisi wote tukaurudilia ukuta, kila mumoja akaendelea na kazi yake.
Basi, malaika wa Yawe aliingia ndani ya kambi ya Waasuria na kuwaua watu elfu mia moja makumi nane na watano. Kesho yake, wakati watu walipoamuka, waliona yale maiti yote.
Petro alipotambua kwamba mambo yaliyotokea ni ya kweli akasema: “Sasa ninajua hakika kwamba Bwana alimutuma malaika wake kuniokoa katika mikono ya Herode na katika mabaya yote Wayuda waliotaka kunitendea.”
Kisha, Daudi na watu wake ambao walikuwa yapata mia sita, waliondoka na kwenda popote walipoweza kwenda. Saulo aliposikia kwamba Daudi amekwisha kimbia kutoka Keila, akaiacha mipango yake yote.