11 Katika kinywa chake kunatokea mienge inayowaka, cheche za moto zinaruka inje.
Kuzimu kuko wazi kabisa mbele ya Mungu. Shimo la kuangamia halina kifuniko chochote.
Maana yeye anaona mpaka kwenye miisho ya dunia, anaona kila kitu chini ya mbingu.
Mungu atapaswa kumwazibu kama unavyoona wewe? Wewe ndiwe unayeamua, wala si mimi. Basi, sema unachofikiri wewe.
Kama wewe ni mwenye haki, unamupatia faida, au yeye anapokea kitu kutoka kwako?
Katika pua yake kunafuka moshi, kama vile chungu kinachochemuka, kama vile nyasi inayowaka.
Yeye anahamisha milima bila yenyewe kutambua, anaipindua mbali kwa hasira yake.
Mbingu ni mali ya Yawe, lakini amewapa wanadamu dunia.
Umemutimizia mapenzi ya moyo wake; wala haukumukatalia ombi lake.
Zaburi ya Daudi. Dunia na vyote vinavyokuwa ndani yake ni vya Yawe; ulimwengu na wote wanaoishi ndani yake ni mali yake.
Kama ningesikia njaa, singekuambia wewe, maana ulimwengu na vyote vinavyokuwa ndani yake ni vyangu.
Sasa basi, kama mukitii sauti yangu na kushika agano langu, mutakuwa watu wangu wachaguliwa kati ya mataifa yote, maana dunia yote ni yangu.
Ni nani anayeweza kumupa Mungu kitu kwanza, kusudi naye apate kumurudishia?”
Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Dunia na vyote vinavyokuwa ndani yake ni vya Bwana.”
Lakini kama mutu akiwaambia ninyi: “Vyakula hivi vimetambikiwa kwa sanamu,” basi musivikule kwa ajili ya yule aliyewaarifu na kwa ajili ya zamiri.
Angalia, mbingu hata mbingu za mbingu ni mali ya Yawe, Mungu wenu, dunia na vyote vinavyokuwa ndani yake.
Muangalie, Sanduku la Agano la Bwana wa dunia yote liko karibu kupita mbele yenu kuelekea muto Yordani.