9 Una nguvu kama mimi Mungu? Unaweza kunguruma kwa sauti kama yangu?
Angeshindana nami kwa nguvu zake zote? Hapana! Bila shaka angenisikiliza.
Musikilize ngurumo ya sauti ya Mungu, na muvumo wa sauti kutoka ndani ya kinywa chake.
Yeye ni mwenye hekima sana na nguvu nyingi. Nani aliyepingana naye, akashinda?
Sauti ya Yawe inasikilika juu ya maji; Mungu mutukufu anapiga radi, sauti ya Yawe inasikilika juu ya bahari!
Sauti ya Yawe ni yenye nguvu, sauti ya Yawe ni yenye mamlaka.
Wewe unaamuru machafuko ya bahari; mawimbi yake yakiinuka, unayatuliza.
Wewe uliumba kaskazini na kusini; milima Tabori na Hermoni inakushangilia.
Zaburi. Mumwimbie Yawe wimbo mupya, kwa maana ametenda mambo ya ajabu! Nguvu yake kubwa, mukono wake mutakatifu umemupatia ushindi.
“Mukono wako wa kuume, ee Yawe, unatukuka kwa nguvu; kwa mukono wako wa kuume, ee Yawe, unawaponda waadui.
Ole kwake mutu anayebishana na Muumba wake: chombo cha udongo kubishana na mufinyanzi wake! Udongo unamwuliza anayeufinyanga: Unatengeneza nini hapa? au kumwambia: Kazi yako si kamili!
Yawe ameonyesha nguvu yake tukufu, mbele ya mataifa yote. Atawaokoa watu wake, na ulimwengu wote utashuhudia.
Ewe Babeli, nilikutegea mutego ukanaswa, wala haukujua kitu juu yake; ulipatikana, ukakamatwa, kwa sababu ulishindana nami Yawe.
Shindo la mabawa ya makerubi iliweza kusikilika hata kwenye kiwanja cha inje, kama sauti ya Yawe wa majeshi anaposema.
Au tunataka kumuchokoza Bwana hata asikie wivu? Munafikiri kuwa sisi tuko na nguvu kuliko yeye?
kusudi watu wote wa dunia wajue kwamba mukono wa Yawe una nguvu; nanyi mupate kumwogopa Yawe, Mungu wenu, milele.”