Basi, mufalme wa Israeli akapeleka waaskari wake karibu na pahali alipoambiwa. Elisha aliendelea kumwonya mufalme naye mufalme alijiweka katika hali ya angalisho. Jambo hilo lilifanyika mara nyingi.
Basi tunajua kama maneno yote yanayosemwa na Sheria, yanawaelekea wale wanaolazimishwa kutii Sheria, kusudi mutu yeyote asikuwe na namna ya kujitetea, na dunia nzima ipaswe kuhukumiwa na Mungu.