Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yobu 4:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Maneno yako yamewainua moyo, umewaimarisha waliokosa nguvu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yobu 4:4
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kila mutu aliyesikia habari zangu alinitakia heri na aliponiona, alikubali habari zile kuwa kweli.


Niliwatangulia kwa kuwaongoza, nikawaonyesha njia. Nilikuwa kwao kama vile mufalme kati ya majeshi yake; kama vile mutu anayewafariji wenye musiba.


Sikiliza! Wewe umewafundisha wengi, na kuiimarisha mikono ya wazaifu.


Lakini sasa shida imekupata nawe unaregea. Imekugusa, nawe unafazaika.


Yawe anawashikilia wote wanaoanguka; anawainua wote waliogandamizwa.


Maneno ya ovyo yanaumiza kama upanga, lakini kusema kwa mwenye hekima kunaponyesha kidonda.


Neno linalosemwa kwa wakati unaofaa, ni kama michoro ya zahabu juu ya feza.


Bwana wetu Yawe amenifundisha jinsi ya kusema, kusudi niwatie moyo wale waliochoka. Kila asubui ananipa hamu ya kusikiliza mambo anayotaka kunifundisha.


Basi, mufalme akabadilika rangi na kufazaika kwa ajili ya mawazo yaliyomufikia, viungo vyake vikaregea na magoti yakaanza kutetemeka.


Basi sasa ni afazali kumusamehe na kumufariji, na kuepuka asikate kitumaini kwa sababu ya huzuni kubwa.


Lakini Mungu anayefariji watu wanyenyekevu, ametufariji kwa njia ya kufika kwa Tito.


Tunawasihi wandugu, muwaonye wale wanaokuwa wavivu, muwatie moyo wale wanaoregea, muwasaidie wale wanaokuwa zaifu, na mukuwe wavumilivu kwa watu wote.


Basi muitie tena nguvu mikono yenu inayopooza, nayo magoti yenu yanayoregea.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ