Yoramu alianza kutawala akiwa na umri wa miaka makumi tatu na miwili; akatawala kule Yerusalema kwa muda wa miaka minane. Wakati alipokufa, hakuna mutu yeyote aliyemusikitikia. Alizikwa katika muji wa Daudi, lakini si katika makaburi ya wafalme.
Usikie maombi yangu, ee Yawe, usikilize kilio changu, usikae kimya ninapolia. Maana, mimi ni kama mugeni tu anayepita, ni musafiri kama vile babu zangu wote walivyokuwa.