Ni nani aliyepanda juu mbinguni na kushuka chini? Ni nani aliyekamata upepo katika mukono? Ni nani aliyefunga maji katika kitambaa? Ni nani aliyeweka mipaka yote ya dunia? Jina lake ni nani? Na ni nani jina la mwana wake? Uniambie kama unajua!
Yawe alitaka shauri toka kwa nani, halafu akapata kuwa mwenye akili? Nani aliyemufundisha kuhukumu kwa haki? Nani aliyemufundisha maarifa, na kumwonyesha namna ya kuwa na akili?
Mungu ndiye aliyeifanya milima, na kuumba upepo; ndiye anayemujulisha mwanadamu mawazo yake; ndiye anayegeuza muchana kuwa usiku, na kukanyaga vilele vya dunia. Yawe wa majeshi ndilo jina lake!
Lakini kwa siku hizi za mwisho amesema nasi kwa njia ya Mwana wake. Mungu alimuweka kuwa murizi wa vitu vyote, na ambaye kwa njia yake aliumba ulimwengu wote.
Anawainua wazaifu toka katika mavumbi, anawanyanyua wakosefu toka katika majivu, na kuwaikalisha pamoja na wakubwa, na kuwarizisha viti vya heshima. Maana, minara ya dunia ni ya Yawe; yeye ameisimika dunia juu ya minara yake.