4 Halafu sauti yake inanguruma, sauti ya Mungu inanguruma kwa utukufu; yeye hazuizi umeme wakati inaposikilika.
Ikiwa haya ni machache tu ya matendo yake, ni minongono tu tunayosikia juu yake, nani anayeweza kujua ukubwa wa nguvu yake?
alipoamua mvua inyeshe wapi, umeme na radi vipite wapi,
Musikilize ngurumo ya sauti ya Mungu, na muvumo wa sauti kutoka ndani ya kinywa chake.
Anafanya uenee chini ya mbingu yote, anaeneza umeme wake katika pembe zote za dunia.
Mungu anapiga radi ya ajabu kwa sauti yake, anafanya mambo makubwa tusiyoweza kuyaelewa.
Una nguvu kama mimi Mungu? Unaweza kunguruma kwa sauti kama yangu?
Yawe alinguruma kutoka mbingu; Mungu Mukubwa akatoa sauti yake.
Enyi falme za dunia, mumwimbie Mungu, mumwimbie Bwana wetu nyimbo za sifa,
Musa akamalizia kwa kusema: “Ee Israeli, hakuna anayekuwa kama Mungu wako, yeye anayeruka toka mbinguni kuja kukusaidia, anapita juu katika anga katika utukufu wake.