Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yobu 32:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Lakini ile roho inayokuwa ndani ya mutu, ile pumzi ya Mungu Mwenye Uwezo, ndiyo inayomwezesha mwanadamu kufahamu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yobu 32:8
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa hiyo mufalme akawauliza watumishi wake: “Huyu mutu ana roho wa Mungu! Tunaweza kumupata mutu mwingine kama huyu?”


Kisha akamwambia Yosefu: “Kwa sababu Mungu amekufunulia haya yote, hakuna mutu mwingine mwenye akili na hekima kama wewe.


basi, sasa ninakutimizia kama ulivyoomba. Ninakupa hekima na akili kwa kipimo ambacho hakuna mutu mwingine aliyepata kuwa nacho mbele yako, na wala hakutatokea mwingine kama wewe nyuma yako.


Watu wote wa Israeli waliposikia juu ya hukumu ya mufalme, walimwogopa. Wakatambua kwamba alikuwa na hekima ya Mungu iliyomuwezesha kutoa hukumu za haki.


Mungu alimupa Solomono hekima zaidi na akili kwa wingi. Maarifa yake yalikuwa kama muchanga wa bahari, hayakukuwa na kipimo.


Lakini hekima na uwezo ni vya Mungu. Yeye ana maarifa na ujuzi.


Yeye ana nguvu na hekima. Wanaodanganywa na wanaodanganya ni wake.


ninaapa kwamba kadiri ninavyoweza kupumua, roho ya Mungu ikiwa bado ndani yangu,


wanaposinzia katika vitanda vyao. Halafu anawafungua watu masikio yao; anawatia hofu kwa maonyo yake,


Roho ya Mungu iliniumba, nayo pumzi ya Mungu Mwenye Uwezo inanipa uzima.


anayetuelimisha kuliko nyama, na kutufanya wenye hekima kuliko ndege!”


Ni nani aliyemujulisha kwarara kujaa kwa muto Nili au aliyemwambia jogoo kwamba mvua inakuja?


Maana Yawe anawapa watu hekima; katika kinywa chake kunatoka maarifa na ufahamu.


Zamiri ya mutu ni taa ya Yawe; inachunguza nafsi ya mutu mpaka ndani kabisa.


Mungu anamujalia mutu anayependezwa naye hekima, akili na furaha; lakini anamupa mwenye zambi kazi ya kuvuna na kulundika, kisha Mungu anavipatia yule anayemupendeza. Hayo nayo ni bure sawa na kutaka kukamata upepo.


Mutu huyo anajua kufanya vile, kwa sababu Mungu wake anamufundisha.


Mungu aliwajalia vijana wale wane maarifa na ujuzi katika elimu na hekima. Zaidi ya hayo, alimujalia Danieli ufahamu wa kufasiria maono na ndoto.


Anabadilisha nyakati na wakati, anaondoa na kuwatawalisha wafalme. Anawapa hekima wenye hekima, anawaongezea wenye maarifa ufahamu.


Basi mutu mumoja anapewa na Roho uwezo wa kusema maneno ya hekima, na mwingine uwezo wa kusema maneno ya ufahamu na Roho yule yule.


Maandiko yote Matakatifu yameandikwa kwa maongozi ya Mungu na yanafaa kwa kufundisha, kuonya, kuhakikisha na kuadibisha katika haki,


Kama mumoja kati yenu akikosa kuwa na hekima, aiombe kwa Mungu ambaye atamupatia. Kwa maana Mungu anawapa watu wote bila upendeleo na kwa moyo mwema.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ