Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yobu 3:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Itawaliwe na giza kubwa sana, mawingu mazito yaifunike. Giza la muchana liitishe!

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yobu 3:5
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Macho yangu ni mekundu kwa sababu ya kulia, kope zangu zimekuwa nyeusi sana,


Kwao wote giza kubwa ni mwangaza wa asubui; wao ni warafiki za vitisho vya giza kubwa.


Wachimba madini wanaleta taa katika giza, wanatafutatafuta mpaka chini zaidi ya udongo, na kuchimbua mawe yenye madini katika giza.


Siku ile ikuwe giza! Na kutoka juu Mungu asijishugulishe nayo, wala mwangaza wowote usiiangaze!


Usiku ule giza kubwa liufunike! Usihesabiwe katika siku za mwaka, usitiwe katika hesabu ya siku za mwezi.


Hakuna weusi wala giza kubwa ambamo watenda maovu wanaweza kujificha.


Umekwisha kuonyeshwa milango ya kifo au kuona milango ya makao ya giza kubwa?


Wengine waliishi katika giza na ukiwa, wafungwa katika mateso na minyororo,


Aliwatoa katika giza na ukiwa, na minyororo yao akaivunjavunja.


Hata nikipita katika bonde la giza kubwa, sitaogopa hatari yoyote, maana wewe, ee Yawe, ni pamoja nami; gongo lako na fimbo yako vinanipa moyo.


Hatujakuasi wewe, wala hatujaiacha njia yako.


Wewe, ee Mungu, umeongoza taifa, umezidisha furaha yake. Watu wanafurahi mbele yako wana furaha kama kwa wakati wa mavuno, kama vile wanaogawanya vitu walivyonyanganya wanavyofurahi.


Mumutukuze Yawe, Mungu wenu, mbele hajawaletea giza, mbele hamujajikwaa miguu kwenye milima inayofunikwa na giza. Ninyi mulitazamia mwangaza, lakini anaugeuza kuwa usiku anaufanya kuwa giza nzito.


Hawakujiuliza hivi: Yuko wapi Yawe aliyetuondoa katika inchi ya Misri, aliyetuongoza katika mbuga, katika inchi ya jangwa na mashimo, inchi inayokauka na yenye giza kubwa, inchi isiyopitiwa na mutu yeyote, wala kukaliwa na mwanadamu?


Kwa hiyo, inchi itaomboleza, na mbingu zitakuwa nyeusi. Maana nimesema nami sitabadilisha nia yangu; nimeamua, wala sitarudi nyuma.


Kwa maana, siku hiyo imekaribia; siku ile ya Yawe iko karibu. Hiyo itakuwa siku ya mawingu ya kutisha, siku ya maangamizi kwa mataifa.


Kama muchungaji anavyowatafuta kondoo wake waliosambazwa, ndivyo nitakavyowatafuta kondoo wangu. Nitawarudisha kutoka kila pahali waliposambazwa kwa siku yenye mawingu ya hatari na giza nene.


Hiyo ni siku ya giza na huzuni; siku ya mawingu na giza nene. Jeshi kubwa linakaribia kama giza linalofunikia milima. Namna hiyo haijapata kuwa hata kidogo wala haitaonekana tena katika vizazi vyote vinavyokuja.


Huyo aliyezifanya nyota zinazoitwa Kilimia na Orioni, ambaye analigeuza giza nene kuwa muchana, na muchana kuwa usiku; yeye anayekusanya maji ya bahari na kuyamwanga juu ya inchi kavu, Yawe ndilo jina lake.


Nitazigeuza sikukuu zenu kuwa kilio, na nyimbo zenu za furaha kuwa maombolezo. Nitawavalisha ninyi wote magunia kwa huzuni na kunyoa vichwa vyenu upaa, kama kuomboleza kifo cha mutoto wa pekee. Na siku ya mwisho itakuwa ya uchungu mukubwa.


Watu hao wanaokaa katika giza, mwangaza umewatokea! Hao wanaoishi katika inchi yenye giza nzito sana ya lufu, wameona mwangaza mukubwa.”


Atawaangazia wale wanaoishi katika giza na wanaokaa katika kivuli cha kifo, kusudi atuongoze tupate kufuata njia ya amani.”


“Basi, mulikaribia na kusimama chini ya ule mulima ambao wakati huo ulikuwa unawaka moto uliofika mpaka mbinguni ukiwa umetanda giza na wingu zito.


Ninyi hamujafikia kwenye kitu kinachoweza kuguswa kama vile Waisraeli walivyofikia kwenye mulima Sinai. Mulima ule uliwaka moto, ulifunikwa na giza nzito, nao ulikuwa na uvumi wa zoruba juu yake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ