16 Kwa nini sikukuwa kama mutoto aliyezaliwa mufu ambaye hakuona mwangaza?
ningepelekwa katika kaburi, na kuwa kama mutu asiyekuwa.
pamoja na wakubwa waliokuwa na zahabu, waliojaza nyumba zao feza tele.
Kule kwa wafu waovu hawasumbui mutu, kule wanaochoka wanapumzika.
Watoweke kama maji yanavyopotelea ndani ya muchanga, kama majani wakanyagwe na kunyauka,
watoweke kama konokono anavyoyeyuka akitembea, kama mimba iliyoharibika isiyoona jua hata kidogo!
Lakini heri zaidi kuliko wafu na wanaokuwa wazima, yule ambaye bado hajazaliwa na kuona maovu yote yanayotendeka hapa chini ya jua.
Mutu akiweza kuzaa watoto mia moja, na akiishi maisha marefu, lakini kama mutu huyo hafurahii maisha yake, wala hafanyiwi mazishi, basi ninasema mutoto aliyezaliwa amekufa ni afazali kuliko mutu yule.
Na kwa mwisho wa wote akanitokea mimi vilevile, mimi ninayekuwa kama mutoto aliyezaliwa pasipo kutimiza miezi.