2 Watu wanachimba chuma ndani ya udongo, wanayeyusha shaba kutoka mawe ya madini.
Naye Sila akazaa Tubali-Kaina, ambaye alikuwa mufuaji wa vyombo vyote vya shaba na chuma. Dada ya Tubali-Kaina alikuwa Nama.
Kwa juhudi kubwa, nimeiwekea akiba nyumba ya Yawe zaidi ya toni elfu tatu za zahabu, zaidi ya toni elfu moja za feza pamoja na shaba na chuma visivyoweza kupimwa maana ni vingi sana. Nimetayarisha mbao na mawe. Lakini utaweza kuongeza.
Hakika kuna nafasi ya kuchimba feza, na pahali ambako zahabu inasafishwa.
Wachimba madini wanaleta taa katika giza, wanatafutatafuta mpaka chini zaidi ya udongo, na kuchimbua mawe yenye madini katika giza.
Zahabu, feza, shaba, chuma, manjanja na madini ya risasi,
Huko mutapata chakula tele na hamutapungukiwa kitu. Mawe yake yana chuma, na kwenye milima yake munaweza kuchimba shaba.