8 Asiyemwogopa Mungu ana tumaini gani wakati Mungu anapokata pumzi yake, anapomwondolea uzima wake?
Lakini waovu macho yao yatafifia, njia zote za kutorokea zitawapotea; tumaini lao la mwisho ni kukata roho!
Uzima wa kila kiumbe, pumzi ya kila mwanadamu, viko katika mikono yake.
Kama nikiweza kwa hiyo nitakuwa nimeshinda, maana mutu mwovu hawezi kwenda mbele yake.
Wote wasiomwogopa Mungu hawatapata watoto, moto utateketeza mahema ya wanaokula kituliro.
mwovu atajiona ameshinda kwa muda tu, furaha ya asiyemwogopa Mungu ni ya muda mufupi tu!
Adui yangu apate azabu ya mwovu, anayesimama kunishambulia aazibiwe kama mubaya.
Hasara haipati watu waovu na maangamizi wale wanaotenda mabaya?
Ndivyo wote wanaomusahau Mungu wanavyokuwa. Tumaini la wasiomwamini Mungu litapotea.
Ni faida gani kwa mutu kupata utajiri wote wa dunia, lakini anapoteza uzima wake? Hakuna kitu mutu anachoweza kutoa kwa kukomboa uzima wake.
“Ole kwenu, ninyi walimu wa Sheria na Wafarisayo, ninyi wanafiki! Munawafungia watu wengine njia ya kuingia katika Ufalme wa mbinguni. Ninyi wenyewe hamwingii mule na zaidi ya hii munawazuiza wale wanaotaka kuingia. [
Ni faida gani kwa mutu kupata utajiri wote wa dunia, lakini anapoteza uzima wake mwenyewe au kujiangamiza?
Tunajua kwamba Mungu hasikilizi maombi ya wenye zambi, lakini anamusikiliza mutu yule anayemuheshimu na kufanya sawa anavyotaka.
Ndipo muliporudi, mukamulilia Yawe, lakini hakuwasikiliza wala hakuwajali.
Wakati huo, ninyi mutalalamika kwa sababu ya mufalme wenu ambaye mumejichagulia ninyi wenyewe. Lakini Yawe hatawajibu.”