Mufalme akamwuliza: “Kijana Abusaloma ni muzima?” Mwetiopia akasema: “Waadui zako, bwana wangu mufalme, pamoja na wote wanaokushambulia wakikutakia mabaya, wakuwe kama huyo kijana Abusaloma.”
Heri kungekuwa mutu wa kunisikiliza! Ninaweza kutia sahihi yangu katika kila neno nililosema. Mungu Mwenye Uwezo anijibu! Heri mashitaki waadui zangu wanayonitolea yangeandikwa!
Sasa bwana wangu, kama vile Yawe anavyoishi na kama vile unavyoishi, unaona kwamba Yawe amekuzuia kulipiza kisasi kwa kumwanga damu na hivyo upate kuwa na kosa. Uwaache waadui zako na wale wote wanaokutakia mabaya wakuwe wapumbafu kama Nabali.