3 ninaapa kwamba kadiri ninavyoweza kupumua, roho ya Mungu ikiwa bado ndani yangu,
Halafu Yawe Mungu akamwumba mwanaume kwa udongo, akamupulizia ndani ya pua pumzi ya uzima, na yule mwanaume akakuwa kiumbe chenye uzima.
Uzima wa kila kiumbe, pumzi ya kila mwanadamu, viko katika mikono yake.
Lakini ile roho inayokuwa ndani ya mutu, ile pumzi ya Mungu Mwenye Uwezo, ndiyo inayomwezesha mwanadamu kufahamu.
Roho ya Mungu iliniumba, nayo pumzi ya Mungu Mwenye Uwezo inanipa uzima.
Usimutumainie mwanadamu, uzima wake ni kama pumzi tu. Yeye anafaa kitu gani?
Yeye hahitaji kushugulikiwa na watu, kama vile angekuwa na lazima ya musaada fulani. Kwa maana yeye ndiye anayewapa watu wote pumzi ya uzima, pamoja na vitu vyote wanavyohitaji.