Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yobu 27:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Kama vile Mungu anavyoishi, aliyeniondolea haki yangu, Mungu Mwenye Uwezo aliyeifanya nafsi yangu ikuwe na uchungu,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yobu 27:2
26 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yoabu akamwambia: “Kama vile Yawe anavyoishi, ungekuwa haujasema jambo lile, hakika watu wangu wangeendelea kuwafuatilia wandugu zao mpaka kesho asubui.”


Basi Elia wa kijiji cha Tisibe katika jimbo la Gileadi akamwambia mufalme Ahabu: “Kama vile Yawe, Mungu wa Israeli, ambaye ninamutumikia, anavyoishi, hakutakuwa umande wala mvua mpaka nitakapotoa amri.”


Elia akamwambia: “Kama vile Yawe wa majeshi anavyoishi, yule ambaye ninamutumikia: leo hii nitajitokeza mbele ya mufalme.”


Alipofika kwenye mulima kwa mutu wa Mungu, akamushika miguu, naye Gehazi akakaribia kusudi amwondoe. Lakini mutu wa Mungu akamwambia: “Umwache, maana ana uchungu mukali, naye Yawe hakunijulisha jambo hilo.”


Ni sawa kwako kunionea, kuzarau kazi ya mikono yako na kupendelea mipango ya waovu?


Mungu amenitia katika mikono ya wapotovu na kunitupa katika mikono ya waovu.


Mujue kwamba Mungu amenitendea vibaya na kuninasa katika wavu wake.


Mungu amefanya moyo wangu uregee, Mungu Mwenye Uwezo amenitia hofu.


Basi, Yobu amesema: “Mimi Yobu sina kosa, Mungu ameniondolea haki yangu.


Yobu, unaona jambo hili ni sawa? Unasema: “Mimi ni mwenye haki mbele ya Mungu.”


Unataka kweli kugeuza hukumu yangu, kuniona nina kosa kusudi wewe usikuwe na kosa?


Yeye ananiponda kwa zoruba, anaongeza vidonda vyangu bila sababu.


Haniachi hata nipumue; maisha yangu anayajaza uchungu.


Enyi watu wa Israeli wazao wa Yakobo, kwa nini munalalamika na kusema: Yawe hatujali sisi! Mungu wetu hajali haki yetu!


Na kama watajifunza mwenendo wa watu wangu kwa moyo wote, wakiapa kwa jina langu, wakisema “Kama vile Yawe anavyoishi”, kama vile walivyowafundisha watu wangu kuapa kwa jina la mungu Bali, basi watastawi katikati ya watu wangu.


ukiapa kwa ukweli, kwa kufuatana na sheria, na kwa haki, kwa kusema “Kama vile Yawe anavyoishi”, halafu mataifa yatapata baraka kutoka kwangu, na kutukuzwa kwa sababu yangu.


Ingawa watu wake wanaapa kwa nafsi ya Yawe, viapo vyao ni vya uongo.


Basi, uwaambie: Kama vile ninavyoishi, –ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe– mimi sikifurahii kifo cha mutu mwovu, lakini ninapenda mutu mwovu aachane na mwenendo wake mubaya, apate kuishi. Mugeuke, muachane na mwenendo wenu mubaya, enyi Waisraeli! Kwa nini munataka kufa?


Lakini kwa kweli, kama vile ninavyoishi na kama vile dunia itakavyojaa utukufu wa Yawe,


Kwa hiyo, kaa hapa usiku wote, na kesho asubui tutaona kama atakubali kukutunza au hapana. Ikiwa atakutunza ni vizuri. Kama vile Yawe anavyoishi, akikataa, mimi nitakutunza. Lala hapa mpaka asubui.”


Kama vile Yawe Mwokozi wa Israeli anavyoishi, hata kama ni mwana wangu Yonatani anapaswa kuuawa.” Lakini hakuna mutu aliyesema neno.


Lakini watu wakamwambia Saulo: “Kwa nini Yonatani, aliyeletea Waisraeli ushindi huu mukubwa, auawe? Haiwezikani hata kidogo. Kama vile Yawe anavyoishi, hata unywele mumoja wa kichwa chake hautaanguka chini. Alichokifanya leo, amekifanya kwa musaada wa Yawe.” Kwa hiyo, watu walimukomboa Yonatani naye hakuuawa.


Nitamutuma mutumishi wangu aende kuitafuta mishale hiyo. Kama nikimwambia: ‘Angalia, mishale hiyo iko upande ule wako, uikamate’, hiyo itakuwa na maana kwamba uko salama, nawe utajitokeza kutoka pahali ulipojificha, maana, kama vile Yawe anavyoishi, kuna amani kwako, na hakuna hatari.


Sasa bwana wangu, kama vile Yawe anavyoishi na kama vile unavyoishi, unaona kwamba Yawe amekuzuia kulipiza kisasi kwa kumwanga damu na hivyo upate kuwa na kosa. Uwaache waadui zako na wale wote wanaokutakia mabaya wakuwe wapumbafu kama Nabali.


Kwa hakika, kama Yawe, Mungu wa Israeli, anavyoishi, amenizuia kukuzuru. Usingefanya haraka kuja kukutana nami, kwa hakika, kesho asubui hakuna mwanaume yeyote wa Nabali ambaye angebaki.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ