2 Watu wanaondoa vitambulisho vya mipaka ya mashamba, na wengine wanaiba makundi ya nyama na kuwafuga.
Basi Wasabea wakatushambulia na kunyanganya nyama na kuua watumishi kwa upanga. Ni mimi tu peke yangu nimepona kwa kuja kukuletea habari.”
Yule naye alipokuwa hajamaliza kusema, mwingine akafika, akasema: “Wakaldea walijipanga makundi matatu, wakashambulia ngamia, wakawatwaa, na wakaua watumishi wako kwa upanga! Ni mimi tu peke yangu nimepona kwa kuja kukuletea habari.”
kwa sababu amewaangamiza wamasikini na kuwaachilia, amenyanganya nyumba ambazo hakuzijenga.
Kama nimeiba shamba ninalolima na kusababisha mifereji yake iomboleze,
Mazao yake yanakuliwa na wenye njaa, hata ngano iliyoota kati ya miiba. Wenye tamaa wananyanganya utajiri wake.
Usiondoe kitambulisho cha mupaka wa zamani, ambacho kiliwekwa na babu zako.
Usiondoe kitambulisho cha mupaka wa zamani, wala usinyanganye mashamba ya wayatima,
Waongozi wa Yuda wamekuwa wenye kubadilisha mipaka ya inchi. Mimi nitawamwangia hasira yangu kama maji.
“Musiondoe kitambulisho cha mipaka ya wajirani zenu, ambayo iliwekwa hapo zamani katika inchi ambayo Yawe wenu anawapatia muirizi.
“ ‘Alaaniwe mutu yeyote anayeondoa kitambulisho cha mupaka wa mwenzake.’ Na watu wote wataitika: ‘Amina!’