4 Unazani anakuazibu na kukuhukumu kwa sababu wewe unamuheshimu?
Ee Mungu, kwa nini unajali hata kumwangalia na kuanza kusamba naye?
Heri mutu angenitetea mbele ya Mungu, kama vile inavyofanyika katika dunia kati ya watu wawili.
Lakini muogope azabu, chuki yenu isiwaletee kifo. Mujue kwamba kutakuwa hukumu!
Unazani kwamba unamufurahisha Mungu Mwenye Uwezo kama wewe ni mwenye haki? Au anapata faida gani kama uko mukamilifu?
Mungu hahitaji kumujulisha mutu wakati wa kumuleta mbele ya tribinali yake.
Mimi ni bahari au nyama mukubwa wa bahari hata upate kuniwekea mulinzi?
Kama ni kushindana, yeye ana nguvu sana! Na kama ni kutafuta juu ya haki, nani atakayemuleta mbele ya tribinali?
Mungu si mutu kama mimi nipate kumujibu, hata tuweze kwenda katika tribinali pamoja.
Usinitie katika hukumu mimi mutumishi wako, maana hakuna yeyote anayekuwa mwenye haki mbele yako.
Usiniazibu tena; ninamalizika kwa mapigo yako.
Wenye nguvu wamenyanganywa, sasa wamelala usingizi wa kifo, washujaa wa vita hawakuweza kutumia mikono yao.
Ulinde kijiti ulichokipanda kwa mukono wako; hicho kichipukizi ulichokomalisha wewe mwenyewe.
Maana, Mungu atahukumu matendo yote, hata yale yanayotendwa kwa siri, yakuwe mazuri au mabaya.
Mimi ninawaonya na kuwaazibu wote ninaowapenda. Basi ufanye nguvu, ugeuke toka katika zambi.