3 Munivumilie, nami nitasema, na nikisha sema muendelee kunichekelea.
Kupapayuka kwako kutanyamazisha watu? Kama ukichekelea watu, hakuna atakayekupatisha haya?
Munyamaze, nami niseme. Kitu kitakachonipata, kinipate.
Akiwachunguza, ninyi mutapona? Au munazani munaweza kumudanganya Mungu kama watu?
Watu wanafungua vinywa vyao na kunichekelea. Makundi kwa makundi wananizunguka na kunipiga makofi kwenye mashavu.
Warafiki zangu wanizarau; ninatoa machozi kumwomba Mungu.
Kweli wanaonichekelea wamenizunguka, matusi yao yananizuiza kulala.
Musikilize kwa uangalifu maneno yangu; na hiyo ikuwe ndiyo faraja yenu.
Lakini ninyi munajua jambo lile vizuri sana! Mbona, basi munasema maneno yasiyokuwa na maana?