Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yobu 2:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Lakini sasa, unyooshe mukono wako umuguse mwili wake. Utaona namna atakutukana waziwazi.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yobu 2:5
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Daudi akamwambia Mungu: “Si mimi ndiye niliyetoa amri watu wahesabiwe? Ni mimi niliyetenda zambi na kufanya uovu. Lakini kondoo hawa wamefanya nini? Ninakusihi sana, ee Yawe, Mungu wangu, mukono wako ukuwe juu yangu na juu ya jamaa ya baba yangu, lakini ugonjwa huu mukali usiwapate watu wako.”


Lakini sasa, unyooshe mukono wako uguse mali yake. Utaona namna atakutukana waziwazi!”


Yawe akamwambia Shetani: “Basi, unaweza kufanya vile unavyotaka juu ya mali yake. Lakini tu yeye mwenyewe usimuguse.” Basi, Shetani akaondoka mbele ya Yawe.


Kila mara karamu ilipomalizika, Yobu aliita wana wake kusudi awatakase. Aliamuka asubui mapema kisha karamu, akatoa sadaka za kuteketezwa kwa moto kwa ajili ya kila mumoja wao maana aliwaza: “Labda wana wangu wametenda zambi na kumutukana Mungu ndani ya mioyo yao.”


Shetani akamujibu Yawe: “Ngozi kwa ngozi! Mutu anatoa kila kitu anachokuwa nacho kusudi aokoe maisha yake.


Yawe akamwambia Shetani: “Basi, unaweza kumufanya vile unavyotaka, lakini usimwue tu.”


Muke wake akamwambia: “Unaendelea kushikilia ukamilifu wako? Umutukane Mungu, ukufe.”


Niko kama bubu, sisemi kitu, kwa maana wewe ndiwe uliyetenda hayo.


Ni watu ambao wananichokoza waziwazi siku zote; wanatambikia miungu yao katika bustani, na kuifukizia ubani juu ya matofali.


Watu watatangatanga katika inchi, wenye kufazaika sana na wenye njaa. Na wakiwa na njaa, watakasirika na kumulaani mufalme wao vilevile na Mungu wao. Wataangalia juu mbinguni


Yule kijana ambaye mama yake aliitwa Selemoti binti ya Dibri wa kabila la Dani, alitukana Mungu na kuzarau jina lake. Basi watu wakamupeleka kijana kwa Musa,


Nawe uwaambie Waisraeli kwamba mutu yeyote atakayemulaani Mungu wake atabeba lazima ya zambi yake.


Kisha nikasikia sauti kubwa kutoka mbinguni, ikisema: “Sasa wokovu, uwezo na ufalme wa Mungu, na mamlaka ya Kristo wake vimefika. Ni vile, kwa yule aliyekuwa akiwashitaki wandugu zetu mbele ya Mungu wetu muchana na usiku ametupwa chini ya mbingu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ