Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yobu 2:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Shetani akamujibu Yawe: “Ngozi kwa ngozi! Mutu anatoa kila kitu anachokuwa nacho kusudi aokoe maisha yake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yobu 2:4
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu wakamuletea Yosefu nyama wao: farasi, ngombe, kondoo, mbuzi na punda, naye akawapa chakula. Mwaka ule Yosefu akakuwa anawapa chakula kwa kubadilishana na nyama wao wote.


Kwa nini sisi tukufe mbele ya macho yako na mashamba yetu yaharibike? Utununue sisi pamoja na mashamba yetu, tukuwe watumwa wa mufalme kusudi tupate chakula. Utupatie ngano tusikufe. Utupatie mbegu kwa ajili ya mashamba yetu.”


Watumishi wake wakamwendea, wakamwambia: “Tumesikia kwamba wafalme wa Israeli ni wema. Basi, uturuhusu tujifunge magunia kwenye viuno na kamba katika shingo, tumwendee mufalme wa Israeli. Labda atayaokoa maisha yako.”


Yawe akamwambia Shetani: “Umemwona vizuri mutumishi wangu Yobu? Katika dunia hakuna mwingine anayekuwa kama yeye. Yeye ni mutu mukamilifu, wa usawa, mwenye kumwogopa Mungu na mwenye kuepukana na uovu. Yeye anadumu katika ukamilifu, ingawa wewe umenisukuma nimwangamize bure.”


Lakini sasa, unyooshe mukono wako umuguse mwili wake. Utaona namna atakutukana waziwazi.”


Ukombozi wa uzima wa mutu ni mali yake, lakini masikini hana njia ya kujikomboa.


Lakini kulikuwa watu kumi katika kundi hilo waliomwambia Isimaeli hivi: Tafazali usituue, maana tuna akiba kubwa ya ngano, shayiri, mafuta na asali ambayo tumeificha katika pori. Basi hao akawaacha wazima.


Ni faida gani kwa mutu kupata utajiri wote wa dunia, lakini anapoteza uzima wake? Hakuna kitu mutu anachoweza kutoa kwa kukomboa uzima wake.


“Ni kwa sababu hii ninawaambia ninyi: musijisumbue kwa ajili ya maisha yenu, kwa ajili ya chakula au kwa ajili ya kinywaji, wala musijisumbue kwa ajili ya miili yenu kwamba mutavaa nini. Uzima ni wa lazima kuliko vyakula, nao mwili ni wa lazima kuliko nguo.


Uzima unapita chakula, nao mwili ni wa lazima kuliko nguo.


Wakamujibu Yoshua: “Tuliambiwa kwamba kwa hakika Yawe, Mungu wenu, alimwamuru mutumishi wake Musa awaangamize wakaaji wote wa inchi hii na kuwapa ninyi inchi hii ikuwe mali yenu. Kwa hivyo, tuliogopea maisha yetu na ndipo tukafanya jambo hili.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ