Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yobu 2:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Yawe akamwambia Shetani: “Umemwona vizuri mutumishi wangu Yobu? Katika dunia hakuna mwingine anayekuwa kama yeye. Yeye ni mutu mukamilifu, wa usawa, mwenye kumwogopa Mungu na mwenye kuepukana na uovu. Yeye anadumu katika ukamilifu, ingawa wewe umenisukuma nimwangamize bure.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yobu 2:3
26 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hizi ndizo habari za Noa na uzao wake. Noa alikuwa mwenye haki na mukamilifu kati ya watu wa wakati ule. Aliishi katika ushirika na Mungu.


Yoabu akamujibu: “Hata kidogo katika maisha yangu! Sina nia ya kuangamiza wala kuharibu.


Kulikuwa mutu mumoja katika inchi ya Usi, aliyeitwa Yobu. Mutu yule alikuwa mukamilifu, wa usawa, mwenye kumwogopa Mungu na mwenye kuepukana na uovu.


Lakini sasa, unyooshe mukono wako uguse mali yake. Utaona namna atakutukana waziwazi!”


Basi, ikatukia siku moja wamalaika wa Mungu walikwenda kukutana mbele ya Yawe. Shetani akakuja kuwa pamoja nao.


Yawe akamwambia Shetani: “Umemwona vizuri mutumishi wangu Yobu? Katika dunia hakuna mwingine anayekuwa kama yeye. Yeye ni mutu mukamilifu, wa usawa, mwenye kumwogopa Mungu na mwenye kuepukana na uovu.”


Mungu aniue akitaka; sina la kupoteza. Hata hivyo nitautetea mwenendo wangu mbele yake.


Yawe akamwuliza Shetani: “Unatoka wapi wewe?” Naye Shetani akamujibu Yawe: “Ninatoka kutembeatembea na kuzungukazunguka katika dunia.”


Shetani akamujibu Yawe: “Ngozi kwa ngozi! Mutu anatoa kila kitu anachokuwa nacho kusudi aokoe maisha yake.


Yeye ananiponda kwa zoruba, anaongeza vidonda vyangu bila sababu.


Ingawa sina kosa, maneno yangu yenyewe yangenihukumu. Ingawa mimi ni mukamilifu, yangehakikisha kwamba mimi ni mupotovu.


Zaburi ya Daudi. Ee Yawe, unitetee, maana nimeishi katika ukamilifu, nimekutumainia wewe bila kusita.


Muangalie mutu mukamilifu, mutu wa usawa; mutu anayependa amani anajaliwa wazao.


Hivyo nitajua kwamba unapendezwa nami, waadui zangu wasipopata ushindi juu yangu.


Mutu wa haki anaokolewa katika shida, na mwovu anaingia mule kwa pahali pake.


Haki inalinda wenye mwenendo sawa, lakini zambi inaangusha waovu.


Mwenye mwenendo sawa anamwogopa Yawe, lakini mupotovu anamuzarau Mungu.


Sadaka ya waovu ni chukizo kwa Yawe, lakini maombi ya watu wa usawa yanamufurahisha Mungu.


Njia ya watu wa usawa ni kujiepusha na uovu; anayechunga njia yake anachunga maisha yake.


Yesu akajibu: “Mutu huyu hakuzaliwa kipofu kwa ajili ya zambi yake wala zambi ya wazazi wake. Lakini amekuwa hivi kusudi matendo ya Mungu yaonekane kwa njia yake.


Sitaki kusema kwamba nimekwisha kufikia mwisho au kwamba nimekwisha kuwa mukamilifu. Lakini ninakaza mwendo kusudi nipate kushinda na kupokea zawadi, kwa maana Yesu Kristo amekwisha kunipokea nikuwe wake.


Heri mutu yule anayevumilia wakati anapojaribiwa, kwa maana akiisha kushinda majaribu, atapokea ile taji ya uzima ambayo Mungu aliahidia wale wanaomupenda.


Majaribu hayo ni kwa ajili ya kupima imani yenu. Zahabu ni kitu kinachoharibika, lakini ingawa vile inapimwa kwa njia ya kuchomwa ndani ya moto. Hivi vilevile imani yenu inayokuwa ya bei kali kuliko zahabu, inapaswa kupimwa kusudi ijulikane kuwa ya kweli. Na kwa sababu hii mutapata sifa, utukufu na heshima wakati Yesu Kristo atakapotokea.


Lakini mukisha kuteswa kwa muda kidogo, Mungu mwenye neema yote aliyewaita kusudi mupate kushiriki naye katika utukufu wake wa milele katika kuungana kwenu na Kristo, yeye mwenyewe atawakamilisha. Atawatia nguvu na kuwasimamisha imara kabisa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ