Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yobu 2:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Warafiki watatu wa Yobu walisikia juu ya hasara zote zilizomupata Yobu, wakaamua kwa pamoja waende kumupa pole na kumufariji. Majina yao ni: Elifasi kutoka inchi ya Temani, Bildadi wa inchi ya Suhi na Zofari wa inchi ya Namati.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yobu 2:11
34 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ketura alimuzalia Abrahamu: Zimurani, Yokisani, Medani, Midiani, Isibaki na Sua.


Wana wa Elifazi walikuwa Temani, Omari, Sefo, Gatamu na Kenazi.


Hawa ndio wakubwa wa makabila yaliyotokana na Esau. Elifazi, aliyekuwa muzaliwa wa kwanza wa Esau alizaa Temani, Omari, Sefo, Kenazi,


Yobabu alipokufa, Husamu wa inchi ya Watemani, akatawala pahali pake.


Watoto wake wanaume na wanawake wakamufikia kwa kumufariji, lakini akakataa kufarijiwa, akisema: “Uniache. Nitaendelea kuomboleza kwa ajili ya mwana wangu, mpaka nitakaposhuka katika kaburi.” Ndivyo baba yake alivyomulilia.


Abrahamu alikuwa na habara aliyeitwa Ketura. Ketura alimuzalia Abrahamu: Simurani, Yokisanu, Medani, Midiani, Isibaki na Sua. Wana wa Yokisanu walikuwa: Seba na Dedani.


Efuraimu baba yao aliomboleza vifo vyao kwa siku nyingi sana, na wandugu zake wakakuja kumufariji.


Kisha Zofari wa inchi ya Namati akamujibu Yobu:


Lakini ninyi munapakaa uongo chokaa, ninyi wote ni waganga wasiofaa kitu.


Kisha Elifasi wa inchi ya Temani, akajibu:


Mambo kama yale nimeyasikia mengi; ninyi ni wafariji wenye kutaabisha!


Warafiki zangu wanizarau; ninatoa machozi kumwomba Mungu.


Kisha Bildadi, wa inchi ya Suhi, akajibu:


Warafiki zangu wakubwa wanachukizwa nami, wale niliokuwa nikiwapenda wamenigeuka.


Munionee huruma, munionee huruma, enyi warafiki zangu; maana mukono wa Mungu umenigusa.


Kisha Elifasi wa inchi ya Temani akamujibu Yobu:


Kisha wandugu zake, wadada zake na warafiki wote waliomufahamu mbele wakamwendea kwake, wakakula chakula pamoja naye. Wakamupa pole na kumufariji kwa ajili ya mateso yote ambayo Yawe alikuwa amemuletea. Kila mumoja wao akamupa Yobu feza na pete ya zahabu.


Yawe alipomaliza kuongea na Yobu, akamwambia Elifasi wa inchi ya Temani: “Kasirani yangu imewaka juu yako na warafiki zako wawili maana hamukusema ukweli juu yangu kama vile mutumishi wangu Yobu alivyofanya.


Basi, Elifasi wa inchi ya Temani, Bildadi wa inchi ya Shua, na Zofari wa inchi ya Namati, wakafanya kama vile Yawe alivyowaambia. Yawe akapokea maombi ya Yobu.


Anayekataa kutendea mema rafiki yake, anakataa kumwogopa Mungu Mwenye Uwezo.


Wasafiri toka Tema wanatafutatafuta, wasafiri toka Sheba wanatumainia.


Halafu Bildadi wa inchi ya Suhi akamujibu Yobu:


Rafiki wa kweli ni rafiki siku zote. Ndugu anazaliwa kusudi asaidie wakati wa taabu.


Warafiki wengi wanaweza kumwangusha mutu, lakini kuna rafiki mwaminifu kuliko ndugu.


Usisahau warafiki zako wala wa baba yako. Ukipatwa na magumu usikimbilie kwa ndugu yako. Afazali jirani ambaye iko karibu kuliko ndugu anayekuwa mbali.


Hasara hizi mbili zimekupata: uharibifu na maangamizi; njaa na mauaji. Nani atakayekuonea huruma? Nani atakayekufariji?


Juu ya Edomu, Yawe wa majeshi anasema hivi: Hakuna tena hekima katika muji wa Temani? Wenye hekima wao hawana shauri tena? Hekima imetoweka kabisa?


Ewe muji wa Temani, mashujaa wako wataogopa na kila mutu juu ya mulima wa wazao wa Esau.


Wayuda wengi walikuwa wamekuja kwa Marta na Maria kwa kuwafariji kwa ajili ya kifo cha kaka yao.


Mufurahi pamoja na wenye kufurahi. Mulie pamoja na wenye kulia.


Kama kiungo kimoja kikiumia, viungo vingine vyote vinaugua pamoja nacho. Kiungo kimoja kikiheshimiwa, viungo vingine vyote vinafurahi pamoja nacho.


Muwakumbuke wale wanaofungwa, mukijisikia sawa vile wenye kufungwa pamoja nao. Vilevile muwakumbuke wale wanaoteswa, mukijisikia sawa vile wenye kuteswa kama wao.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ