9 Amenivua utukufu wangu; ameiondoa taji yangu juu ya kichwa.
Anawatembeza washauri miguu wazi, anawafanya waamuzi kuwa wapumbafu.
Anaacha makuhani watembee uchi; na kuwaangusha wenye nguvu.
Nimejishonea nguo za gunia; utukufu wangu nikautupa katika mavumbi.
Lakini sasa watu wananichekelea, tena watu wanaokuwa wadogo kuliko mimi; watu ambao niliwaona baba zao hawafai hata kuwahesabu kama imbwa wangu wakilinda kondoo.
Lakini sasa, ee Mungu, umemutupa na kumukataa, umejaa kasirani juu ya huyo uliyemuchagua.
Umefuta agano ulilofanya na mutumishi wako; umeitupa taji yake ya kifalme ndani ya mavumbi.
Umepoteza ukali wa silaha zake; ukamwachilia ashindwe katika vita.
Maana utajiri haudumu milele, wala taji haidumu kwa vizazi vyote.
Nanyi mutaitwa: “Makuhani wa Yawe”, Mutaitwa: “Watumishi wa Mungu wetu”. Mutafaidika kwa utajiri wa mataifa, mutatukuzwa kwa mali zao.
Taji tuliojivunia imeanguka. Ole kwetu maana tumetenda zambi!
Utukufu wa Efuraimu utatoweka kama ndege; watoto hawatazaliwa tena, hakutakuwa watoto wa kuzaliwa, wala hakutakuwa atakayepata mimba!